Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 25 Januari 2015

DRC;KIPENGELE CHA UTATA CHATOKA

Maandamano ya KInshasa ya jula lilopita
Bunge la wawakilishi la Jamhuri ya Demokrasi ya Congo limepitisha mswada uliorekibishwa kuhusu uchaguzi, baada ya kuondoa kipengee kilicholeta utata, na ambacho upinzani unasema kingerefusha awamu ya uongozi wa Rais Kabila.
Mswada ulivyopitishwa awali juma lilopita ulizusha maandamano ya siku kadha.
Mashirika ya kutetea haki za kibinaadamu yanasema watu 40 walikufa katika maandamano hayo.
Mswada wa awali ulitaka kufanywe sensa kabla ya uchaguzi wa rais - upinzani uliona kuwa hiyo itachelewesha uchaguzi wa rais ambao umepangwa kufanywa mwaka ujao.
CHANZOBBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni