Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 31 Januari 2015

SAUDIA YAAHIRISHA VIBOKO VYA MWANABLOGU


Maandamano ya Raif Badawi
Mamlaka nchini Saudi Arabia kwa mara nyengine tena imeahirisha adhabu nyengine ya viboko dhidi ya mwanablogu Raif Badawi.
Hakuna sababu iliotolewa,lakini awamu mbili za kutoa adhabu kama hiyo hapo awali ziliahirishwa kutokana na sababu za kiafya.
Bwana Badawi amepewa hukumu ya viboko 1000 pamoja na kuhudumia kifungo cha miaka 10 jela kwa kutusi Uislamu.
Raif Badawi na familia yake
Mwanaharakati wa Saudia ambaye pia ni wakili Suad al Shammary ambaye alifanya kazi na bwana Badawi katika blogi yake ameachiliwa huru.
Alizuiliwa kwa miezi mitatu bila kufunguliwa mashtaka kuhusu matamshi aliotoa katika mtandao wa Twitter ambayo wapinzani wake walisema yanapinga Uislamu.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni