Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 25 Januari 2015

ANDY MURRAY AMBWAGA GRIGOR DIMITROV


Andy Murray
Mcheza Tennis maarufu Andy Murray amembwaga Grigor Dimitrov katika kusaka kibali cha kushiriki mashindano ya wazi ya mchezo wa Tennis ya Australia.
Mshindi huyo wa mchezo wa Tennis Uingereza Murry aliibuka mshindi baada ya kujipatia pointi 6-4 6-7 (5-7) 6-3 7-5 ndani ya saa tatu na dakika 32.
Katika seti ya tano ya mchezo huo dalili za ushindin wa Murray zilianza kuonekana na kisha ushindi huo kudhihirika wazi katika michezo mitano ya mwisho.
Kwa ushindi huo sasa Andy Murray anatarajiwa kukwaana na raia wa Austaralia Nick Kyrgios katika mzunguko wake wa nane.
Murray atakuwa akicheka robo fainal ya 16 katika mashindano Grand Slam ikiwa ndiyo hatua ambayo alimtoa Dimitrov katika michuano ya Wimbledon mwakajana.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni