Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 24 Januari 2015

THE EASAFERICAN LAPIGWA MARUFUKU





Serikali ya Tanzania imepiga marufuku kuchapishwa na kusambazwa kwa gazeti la kila wiki la The EastAfrican kwa madai ya kuwa halijasajiliwa nchini humo.
Hata hivyo Wilfred Kiboro, mwenyekiti wa kampuni ya Nation Media Group, wachapishaji wa gazeti hilo la lugha ya kiingereza, ameeleza kuwa adhabu hiyo haikutarajiwa na wala haistahili na kubainisha kuwa wamekuwa wakisambaza gazeti hilo Tanzania kwa miaka 20 bila matatizo.
Kampuni ya Nation imedai sababu kubwa huenda ni serikali ya Tanzania kutofurahishwa na msimamo wake wa kuandika habari dhidi ya maovu kama rushwa na kero nyingine nchini Tanzania.
Kampuni hiyo imesema serikali ya Tanzania imetaja kutofurahishwa na kibonzo kilichochapishwa katika toleo la wiki hii, ambapo imesema kimemdhalilisha Rais Jakaya Kikwete.
Hata hivyo BBC haikuweza kumpata afisa wa serikali ya nchi hiyo anayehusika na usajili wa magazeti kuweza kutoa maelezo zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni