Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 28 Januari 2015

AMNESTY YAKOSOA JESHI LA NIGERIA


Wakuu wa jeshi la Nigeria
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu, Amnesty International, limelishutumu jeshi la Nigeria kwa kushindwa kuwalinda raia katika mji wa Baga uliopo kaskazini mashariki mwa Nigeria, licha ya kuwepo onyo kwamba wanamgambo wa Boko Haram wangelitekeleza shambulio.
Linanukuu duru ambayo haikutajwa jina aliyesema kwamba wanamgambo hao waliwaambia wakaazi miezi miwili awali kwamba walikuwa wanapanga shambulio.
Amnesty International linasema waanjeshi walitazama tu jinsi vikosi vya Boko Haram vilivyokuwa vikiongezeka. Inakadiriwa kwamba kati ya watu 150 hadi 2000 waliuawa katika shambulio hilo lililotokea mapema mwezi huu.
Shirika hilo linadai kwamba limeelezea wasiwasi wake mara kadhaa awali kwamba vikosi vya usalama haviwajibiki vya kutosha kuwalinda raia dhidi ya unyanyasaji na ukiukaji wa haki za binaadamu unaotekelezwa na Boko Haram.
Tangu mwaka 2009, Boko Haram limekuwa likiwalenga raia na kufanya uvamizi, kuwateka raia na mashambulio ya mabomu, huku mashambulio yao yakiongezeka kwa idadi na ukubwa. Malefu ya watu wameuawa katika mashambulio hayo, mamia kutekwa na maelfu wengine wameachwa bila makaazi baada ya kulazimika kutoweka mapigano.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni