Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 28 Januari 2015

KORTI YA KWANZA GOOGLE,YAHOO NA MICROSOFT

Mahakama kuu nchini India imeamrisha kampuni kubwa za internet, Google, Yahoo na Microsoft kubana matangazo ya biashara ya kuwapima wanawake wajawazito ili kubaini jinsia ya mtoto kabla ya kuzaliwa.
Matangazo kama hayo, ni kinyume na sheria nchini India kwa sababu kuna visa vingi vya wanawake kuavya mimba wanapogundua wana mtoto mwenye jinsia wasioitaka.
Hali hii imechochea tatizo la pengo katika jinsia moja kuwa ikilinganishwa na nyingine.
Mahakama ilikuwa inatoa uamuzi katika kesi iliyowasilishwa mbele yake kuhusu kuzagaa kwa matangazo ya biashara ya kubaini jinsia ya mtoto akiwa tumboni kwenye mitandao hio.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni