Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 18 Januari 2015

WATU 5,WAUAWA KUFUATIA MAANDAMANO NIGER


Maandamano Niger
Watu watano wameuawa kwenye mji mkuu wa Niger, Niamey ikiwa ni siku ya tatu ya maadamano ya kupinga kuchapishwa kwa kibonzo cha mtume Mohammed na gazeti la kila wiki nchini Ufaransa la Charlie Hebdo.
Karibu vijana 1000 waliokuwa wamebeba chuma na shoka waliandamana kwenye barabara za mji huo wakiwarushia polisi mawe ambapo walijibu kwa kurusha vitoa machozi.
Waandamanaji hao walichoma moto karibu makanisa 7 mjini Niamey.
Maiti mbili zilizokuwa zimekatwakatwa zilipatikana ndani ya kanisa moja lililokuwa limeteketezwa moto.
 Maandamano Niger
Picha za runinga zilionyesha waandamanaji wakirarua biblia wakisema Allahu Akbar huku wakipeperusha Koran.
Baadhi ya biashara za Ufaransa nazo zilivamiwa yakiwemo maduka ya kampuni ya simu ya Orange.
Ubalozi wa Ufaransa nchini humo umewashauri raia wake walio mjini Niamey kusalia majumbani mwao.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni