Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 19 Januari 2015

SENEGAL YAIBWAGA GHANA


Senegal yaichapa Ghana
Mshambuliaji wa Senegal Moussa Sow alifunga bao la mda wa lala salama na kuisaidia Senegal kupata ushindi dhidi ya Black stars ya Ghana.
Mchezaji huyo aliyeingia dakika za mwisho za mechi hiyo alifunga bao lake kunako dakika ya 90 na kuipatia timu yake alama zote tatu.
Mchezaji wa Ghana Andrew Ayew alifunga mkwaju wa Penalti baada ya kiungo wa kati wa Everton Christian Atsu kuangushwa katika eneo la hatari.
Lakini Senegal ilijitahidi na kupiga chuma cha goli la Ghana kupitia mchezaji Kara Mbodj,kabla ya mshambuliaji wa Stoke Mame Biram Diouf kufunga bao la kusawazisha huku Mousa Sow akifunga bao la Ushindi.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni