Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 18 Januari 2015

AFCON;KUNDI B,LASHINDWA KUTOA MBABE


Kundi B katika michuano ya kombe la mataifa ya Afrika lenye timu za Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Tunisia na Cape Verde limeshindwa kuibua mbabe baada ya timu zote kutoka sare ya kufungana bao 1-1.
Katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo Zambia iliumana na majirani zake Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, ambapo Zambia iliweza kujipatia bao la mapema ikiwa ni katika dakika ya pili lililofungwa na Given Singuluma na kudumu hadi mapumziko. Hata hivyo Yannick Bolasie aliweza kuisawazishia timu yake ya DR Congo katika dakika ya 66. Hadi kipenga cha mwisho kinapulizwa timu zote zilikuwa zimeambulia goli moja na pointi moja.
Timu ya Tunisia ilivaana na Cape Verde katika mchezo wa pili wa kundi B. Walikuwa ni Tunisia walioanza kujipatia bao katika dakika ya 70 likifungwa na Ali Moncer. Lakini dakika saba baadaye Cape Verde ilisawazisha kupitia mkwaju wa penalti uliofungwa na Almeida Ramos. Mchezo huu nao ulimalizika kwa sare ya 1-1, hivyo kutokuwepo mbabe wa kundi.
Leo ni mechi za kundi C ambapo Ghana itaonyeshana kazi na Senegal, zikifuatiwa na mchezo kati ya Algeria na Afrika Kusini.
Kundi A linaongozwa na timu ya Gabon ambayo iliirarua Burkina Faso 2-0 katika mchezo wa Jumamosi, huku wenyeji Equatorial Guinea wakitoka sare ya 1-1 na Congo.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni