Waandamanaji Misri
Serikali ya Misri imesema watu kumi
na wanane akiwemo Polisi mmoja wameuawa wakati wa maandamano
yaliyofanyika nchini humo wakati wakiadhimisha miaka minne tangu
kuangushwa utawala wa Hosni Mubarak.
Vifo hivyo vimetokea mjini
Alexandria na cairo,Serikali ilipiga marufuku kuadhimisha kumbukumbu
hizo hali iliyosabbaisha vurugu kati ya Waandamanaji na Polisi.Zaidi ya watu 400 pia wanashikiliwa kutokana vurugu hizo.Hata hivyo serikali ilipiga marufuku tukio hilo linalodaiwa kuwa ni la kumbukumbu ya maandamano 2011.
Maandamano hayo ya mwaka 2011 nchini Misri yalikuwa yakiratibiwa na makundi ya Waislam wenye msimamo mkali ambapo vikosi vya usalama vilishindwa kuwadhibiti waandamanaji hao
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni