Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 25 Januari 2015

EBOLA NI FUNZO KUBWA KWA WHO DUNIANI


Mkurugenzi mkuu wa WHO, Margaret Chan


Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, WHO, ameeleza mpango wa kuliimarisha shirika hilo baada ya malalamiko mengi kuhusu namna WHO ilivyoshughulikia mripuko wa Ebola Afrika Magharibi, ambayo imeuwa watu zaidi ya 8,000.

Margaret Chan alielezea mripuko huo kuwa maafa ambayo ni funzo kubwa kwa ulimwengu na WHO.
Katika kikao cha viongozi wa WHO mjini Geneva, Bibi Chan alisema mbinu za kupambana na misukosuko kama hiyo zinafaa kuimarishwa na kuanzishwe mfuko wa kugharimia hali ya dharura.
Alisema maafa ya Ebola yameonesha piya kwamba mfumo mwema wa afya wa taifa ni kitu cha lazima, siyo anasa.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni