Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 13 Januari 2015

KORT YABATILISHA UAMUZI DHIDI YA MUBARAK


Hii ndio kesi pekee iliyokuwa imesalia dhidi ya Mubarak
Mahakama nchini misri imebatilisha uamuzi wake kuhusiana na tuhuma za uproraji wa mali ya umma zilizokuwa zinamkabili aliyekuwa Rais wa wa nchi hio, Hosni Mubarak, na wanawe wawili.
Mahakama hio sasa inasema kesi hio itaanza kusikilizwa upya. Mahakama imemeelezea kuwa imegundua mikakati ya kisheria haikufuatwa.
Uamuzi huo una maana kwamba Mubarak ataondolewa katika hospitali ya kijeshi ambako anazuiliwa kwa mujibu wa wakili wake. Hio ndio kesi iliyoyokuwa imesalia mahakamani dhidi yake.
Mnamo mwezi Mei mwezi jana, Mubarak alikuwa emehukumiwa jela miaka mitatu kwa kupora mamilioni ya dola pesa ambazo zilinuiwa kuikarabati ikulu ya Rais.
Wanawe Mubarak, Gamal na Alaa,walifungwa jela miaka minne wakati hukumu ilipotolewa dhidi ya babao.
Tuhuma nyinginezo dhidi ya Mubarak ya kuamrisha mauaji ya waandamanaji mwaka 2011 wakati wa mapinduzi ya kiraia, zilitupiliwa mbali mwezi Novemba mwaka jana.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni