Waandamanaji Ufaransa
Mfalme wa Jordan na Rais wa
Palestinian Mahmoud Abbas ni baadhi ya viongozi kutoka Mashariki ya kati
walioshiriki katika maandamo yaliyofanyika mjini Paris Ufaransa kulaani
shambulio la kigaidi lililofanyika.
Morocco haijawasilisha
uwakilishi wa salam za rambi rambi kutokana na msimamo wake tofauti na
mwenendo wa Gazeti la Charlie Hebdo kutokana na vibonzo ambavyo vimekuwa
vikichorwa hasa vile vinavyolenga masuala ya kidini.Rais Hollande aliungana pia na Waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu,katika Sinagogi la Grand kuomboleza kwaajili ya waathirika wane wa shambulizi la kigaidi katika Supermarket . Netanyahu alimshukuru mmiliki wa Supermarket iliyoshambuliwa Lassana Bathily kwa jitihada zake katika kuwaokoa mateka waliokuwa ndani ya jingo hilo.
chanzo bbc
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni