Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 5 Januari 2015

MITANDAO YAKATAA UBAGUZI UBAGUZI WA KIDINI


Mtu anayetumia mtandao wa facebook kwa mawasiliano
Mitandao ya Twitter na facebook imekataa kuchapisha mamia ya jumbe za chuki licha ya kutakiwa kuchapisha jumbe hizo na makundi ya ubaguzi .
Kulingana na uchunguzi uliofanywa na gazeti la The Independent nchini Uingereza, idadi ya jumbe baadhi yao zikiwa zinawashtumu waislamu kwa kuwa wabakaji na kuwafananisha na ugonjwa wa saratani zimeongezeka kwa kiwango kikubwa katika kipindi cha miezi iliopita baada ya kashfa ya unyanyasaji wa kijinsia katika eneo la Rotherham na mauji ya mateka wa Uingereza yaliofanywa na kundi la Isis.
Facebook imesema kuwa iliamua kuzingatia usawa kati ya uhuru wa kujieleza na kuimarisha mazingira yalio salama,lakini pia ikasema kuwa haitakubali kuchapisha jumbe zinazowaingilia watu wengine kutokana na rangi au dini.
Twitter kwa upande wake imesema kuwa inazipitia jumbe zote zinazokiuka sheria zake zinakataa matamshi yoyote yanayoweza kuzua vurugu.
CHANZO  BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni