Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 6 Januari 2015

MWANA WA MFALME KUWANIA URAIS FIFA


Blatter(kushoto) na Ali Bin Al Hussein (Kulia)
Makamu wa Rais wa shirikisho la soka duniani, Mwanamfalme Ali Bin Al Hussein wa Jordan, amesema kuwa atamenyana na Sepp Blatter kuwania urais wa shirikisho hilo.
Ali Bin Al Hussein amesama atagombea urais wa shirikisho hilo katika uchaguzi utakaofanyika mwezi Mei.
Sepp Blatter anawania urais wa shirikisho hilo kwa muhula wa tano.
Kwa upande wake, Ali Bin Hussein, huenda akapokea uungwaji mkono wa mashirikisho ya soka Ulaya ingawa haijabainika ikiwa ataungwa mkono na shirikisho lenye nguvu sana la soka ya Bara Asia.
Mwanamfalme huyo, amesema ni wakati sasa wa kubadilisha mambo katika shirikisho hilo hasa kutokana na kashfa nyingi ambazo zimekumba soka duniani.
Alikuwa akigusia madai ya rushwa ambayo amehusishwa nayo, bwana Blatter na kutikisa uongozi wake wa shirikisho hilo kwa miaka 17 iliyopita.
Mwanadiplomasia wa Ufaransa Jerome Champagne, pia anajiandaa kuwania uongozi huo dhidi ya wawili hao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni