Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 12 Januari 2015

SOMO LA LE;ATHARI ZA UTOAJI MIMBA





Tatizo la utoaji mimba hapa nchini ni kubwa
sana ingawa bado utafiti unaendelea
kufanyika.
Imegundulika kuwa kati ya mimba 100
zinazoharibika, 80 zinatokana na wanawake
‘kuzichokonoa’ wenyewe na hizi ndizo
ninazozizungumzia.
Zile mimba ambazo zinaharibika zenyewe,
wahusika wanapofika hospitalini
husafishwa na wengine wanalazimika
kufanyiwa upasuaji na maisha yakaendelea
bila tabu.
Kadhalika katika wodi ya dharura ya
wanawake imegundulika kuwa nusu ya
idadi ya mimba zimeharibika kwa kutolewa
kienyeji.
Kati ya watoto 100,000 wanaozaliwa, 454
hufa kutokana na uchokonolewaji
(abortion) wa mimba ambao ni sawa na
asilimia 16-19, na hufuatiwa na vifo.
Madhara ya utoaji mimba
Madhara yanayoambatana na utoaji mimba
ni vifo, kupoteza damu nyingi, kifafa cha
uzazi na maambukizi hatarishi katika mfuko
wa uzazi au mirija ya uzazi.
Haya yote yanaambatana na homa kali na
maumivu makali, kutunga usaha kwenye
kizazi na kulazimika kufanyiwa upasuaji wa
dharura au haraka kitaalamu; kikubwa mara
nyingi ni kifo.

Mhusika kama akipona kutokana na athari
ya kuichokonoa mimba visivyo au kwa
nguvu sana, wakati mwingine husababisha
uharibifu wa mfuko wa uzazi na mirija yake,
na hubakiwa na makovu kwenye ile ngozi
laini ya mfuko wa uzazi, ambayo
humsababishia maumivu makali
anapokaribia siku zake za hedhi ama
kuupoteza mzunguuko wake.
 
Hii ni kwa
muda mrefu au milele. Kitaalamu wanaita ni
kupoteza heshima ya uzazi (quality of life).
Athari nyingine ni kufungwa kwa kizazi,
kwamba mirija ya uzazi ikijifunga basi
mwanamke huyo hawezi tena kuzaa
maishani mwake.
Kutokana na kujifunga kwa mirija ya uzazi,
athari ni kuwa mbegu ya yai la mwanaume
ambayo ni ndogo hujipenyeza na kuingia,
na mbegu ya yai la mwanamke ambayo ni
kubwa hupita na yanapokutana kusabibisha
mimba kutunga nje ya kizazi, ambayo
kitaalamu huitwa “ectopic pregnancy”.
Kwa kuwa mimba hiyo iko nje ya mazingira
ya kawaida, inaweza ikapasuka na kupoteza
damu nyingi na kusababisha kifo na
ikiwahiwa ni kufanyiwa upasuaji na
kulifunga eneo hilo.
Athari nyingine ni ugumba ambao kitaalamu
unajulikana kama “infertility”. Hali hii
inatokana na uharibifu wa mazingira ya
mpango wa mfuko wa uzazi na hasa kwa
uchokonoaji wa mimba, hivyo kufungwa
kwa kizazi, pengine hedhi inakoma na kwa
kutopata hedhi wanawake wengi
huchanganyikiwa.
Tatizo hili la ugumba huwa linasababishwa
na kukwanguliwa kwa ile ngozi laini
inayozunguka tumbo la uzazi.
Kukwanguliwa huko kunatokana na ama
vifaa vinavyotumiwa kuichokonoa mimba
hiyo au madawa makali.
Athari nyingine kama uchokonoaji umepita
kiasi na kufikia kwenye utumbo mkubwa
huathirika na kusababisha utumbo
kutobolewa na kuwekwa mrija wa kutolea
choo kikubwa.
Vile vile hali hiyo usababisha ugandaji wa
damu kwenye mishipa ya fahamu kuelekea
kwenye ubongo. Hii ni hatari mno, kwani
inasababisha mhusika kuwa na hali kama ya
kiharusi.

MC.RAY
WHATSAPP 0659/375263
INSTAGRAM MC.RAYMONDMUSHI
FACE BOOK Raymond Mushi
PAGE Rayshughuli



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni