Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 13 Januari 2015

UBANI WA MTOTO WAMTIA MATATANI MTOTO



Mtoto huyo inaarifiwa aliiba pakiti ya bigjii na kukosa kufika mahakamani mara mbili
Kiongozi mmoja wa mashitaka katika jimbo la Idaho nchini Marekani, alitoa kibali cha kukamatwa kwa mtoto mwenye umri wa miaka 9 ambaye alikosa kufika mahakamani kama alivyotakiwa.
Kituo kimoja cha televisheni nchini humo KHQ-TV kimeripoti kwamba mtoto huyo mvulana alifikishwa mahakamani kwa kuiba paketi ya gamu/bigiji/chingamu/ au ubani wa kutafuna .
Polisi wanasema kuwa ni mara ya kwanza kwa miaka 30 kwa kibali cha kukamatwa kutolewa kwa mtu mwenye umri mdogo kama huo.
Inaarifiwa mtoto huyo alikosa kufika mahakamani kwa sababu jamaa wake walikosa uwezo wa kumpeleka mahakamani humo na kwa sababu ya umri wake mdogo asingeweza kuendesha gari.
Hata hivyo mwendesha mkuu wa mashitaka Barry McHugh, alisema alilazimika kutoa kibali cha kukamatwa kwa mtoto huyo kwa sababu ni mara yake ya pili kukosa kufika mahakamani.
Hata hivyo alisema hawezi kuzungumzia tena kesi hio kwa sababu inamhusu mtu aliye chini ya umri wa miaka 18.
Mtoto huyo kwa sasa amezuiliwa katika kituo cha watoto wakorofi.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni