Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 11 Januari 2015

AFISA WA KANISA APIGWA RISASI MOMBASA


Kanisa
Polisi nchini Kenya wanasema afisa mmoja wa kanisa amepigwa risasi na kuuawa alipokuwa akielekea katika maombi.
Madhumuni ya mauaji hayo hayajatambulika, lakini Muungano wa Makanisa mjini Mombasa tayari umesema ni mauji ya kidini.
Mauaji ya afisa wa kanisa jijini Mombasa yanatishia kuhangaisha wakaazi walioanza mwaka kwa amani baada ya machafuko mengi ya mwaka 2014.
Polisi wanasema afisa wa kanisa moja jijini Mombasa alipigwa risasi na kufariki alipokuwa akiingia ndani ya shule moja ambayo wameikodisha kufanya maombi yao.
Polisi Mombasa
Mkuu wa Upelelezi wa Uhalifu Mombasa Ondiek amesema mtu mmoja aliyekuwa na bunduki alimfuata jamaa huyo hadi akaingia ndani ya uwanja wa shule kabla ya kumpiga risasi. Alikufa papo hapo.
Aidha Ondiek amesema Polisi waliokuwa wameshika doria shuleni walisikia sauti za risasi na hivyobasi kumkabili muuaji huyo, lakini akahepa ndani ya vitongoji vilivyo karibu na shule.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni