Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 11 Januari 2015

KILEVI;WATU ZAIDI YA 50,WAFA MSUMBIJI


Mwanamke aliyetengeneza bia ni miongoni mwa waliopoteza maisha
Serikali nchini Msumbiji imetangaza siku tatu za maombolezo nchi nzima baada ya zaidi ya Watu 50 kupoteza maisha baada ya kunywa kilevi kinachoelezwa kuwa na sumu.
Watu hao walikunywa kilevi hicho wakiwa msibani.
Watu wengine kadhaa waliokunywa kinywaji hicho siku ya jumamosi walikimbizwa hospitalini.
Maafisa wanasema wanaamini kuwa kilevi hicho cha kienyeji kilichotengenezwa kwa mtama na mahindi kilikuwa na sumu ya nyongo ya mamba wakati waombolezaji walipokuwa makaburini.
Sampuli za damu za walioathirika na pombe hiyo pamoja na sampuli za bia zimepelekwa mji mkuu wa nchi hiyo, Maputo kwa ajili ya uchunguzi.
Mwanamke aliyetengeneza pombe hiyo sambamba na nduguze ni miongoni mwa waliopoteza maisha.uchunguzi kuhusu tukio hilo unafanyika.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni