Wapiganaji wa kundi la Alshabaab wamedai kuwaua wapelelezi wanne wa Marekani nchini Somali
Wapiganaji wa kundi la Alshabaab
kutoka Somalia wanasema kuwa wamewaua watu wanne wanaodaiwa kuwa
wapelelezi wa Marekani,Ethiopia na serikali ya Somalia.
Wanne hao
wanadaiwa kupigwa risasi katika mji wa Baradhere siku ya jumanne baada
ya jaji mmoja wa Alshabaab kuwapata na hatia ya kuwaunga mkono
wapelelezi wa CIA na mashirika yanayokabiliana na kundi hilo.Wiki iliopita maafisa wa Somali wanasema kuwa shambulizi moja la ndege lililotekelezwa na Marekani lilimuua kiongozi wa ujasusi wa Alshabaab Abdishakur Tahlil.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni