Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 4 Januari 2015

ISRAEL KUSITISHA MSAADA KWA PALESTINA


Waziri mku nchini Israel benjamini Netanyahu 
Maafisa nchini Israel wanasema kuwa serikali hiyo itasimamisha fedha kwenda kwa utawala wa Palesina siku moja baada ya utawala huo kutuma ombi la kutaka kuwa mwanachama wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita.
Maafisa ambao hawakutajwa walisema kuwa baraza la mawaziri nchini Israeli limeamua kuzuia kutolewa kwa dola milioni 125 ambazo hutumiwa kuendesha shughuli za serikali ya utawala wa Palestina.
Hatahivyo afisa kutoka utawala huo (Saeeb Erekat) ameitaja hatua hiyo ya Israeli kama adhabu iliyo kinyume na sheria.
Ikiwa utawala wa Palestina utafanikiwa kujiunga na mahakama ya ICC itasababisha Israeli kufikishwa mbele ya mahakama hiyo kutokana na uhalifu kwenye sehemu inazokalia.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni