Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 11 Januari 2015

MAANDALIZI;KOMBE LA MATAFA YA AFRIKA



Timu ya Taifa ya DRC itakayoshiriki Kombe la Mataifa ya Afrika 
Mlinzi wa Orlando Pirates Ayanda Gcaba ameitwa kwenye timu ya taifa ya Afrika Kusini Bafanabafana ili kuziba nafasi ya Patrick Phungwayo.
Bafanabafana inashiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika michuano itakayoanza Januari 17 mwaka huu.
Phungwayo ambaye naye ni mchezaji wa Orlando Pirates alilazimika kurudi nyumbani baada ya kupata majeruhi ambayo hayatamwezesha kuitumikia timu yake ya taifa.
Kocha wa Bafana bafana Epharaim Shakes Mashaba amesema amesikitishwa kwa kumkosa Phungwayo lakini ameonyesha kuwa na matumaini na mbadala wa mchezaji huyo Ayanda Gcaba
wakati huo huo mashabiki wa timu ya taifa ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo nayo itashiriki mashindano hayo wamekuwa na matumaini ya timu yao kufanya vizuri na hata kunyakua kombe hilo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni