Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 7 Januari 2015

MKIA WA NDEGE AIR ASIA WAPATIKANA


Mkia wa Ndege wa Air Asia umepatikana bahari ya Java
Mkia wa ndege ya Air Asia iliyoanguka umepatikana kwenye bahari ya Java, kikosi cha kilichokuwa kikisaka ndege hiyo kimeeleza.
Mkia huo wa ndege hutunza visanduku vyeusi vinavyorekodi mawasiliano ndani ya ndege ambavyo vingeweza kuwasaidia wachunguzi kubaini chanzo cha ajali.
Sehemu hiyo ya mabaki ya ndege ilionekana kwenye eneo la ziada lililoongezwa kwenye operesheni ya kutafuta ndege hiyo.
Air Asia ilipotea ilipokuwa ikitoka Surabaya, Indonesia kwenda Singapore tarehe 28 mwezi Desemba ikiwa na Watu 162.
Hakuna manusura yeyote aliyepatikana.
Mpaka sasa miili 40 pekee imepatikana lakini Mamlaka zinaamini kuwa abiria wengi zaidi wamenasa ndani ya ndege hiyo.
chanzo bbc.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni