Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 7 Januari 2015

PALESTINA KUWA MWANACHAMA WA ICC


Mahakama ya kimataifa kuhusu Uhalifu wa kivita ICC
Umoja wa mataifa umedhibitisha kuwa Palestina itakuwa mwanachama wa mahakama ya kimataifa ya ICC iliyo chini ya amri ya Roma kuanzia tarehe 1 mwezi Aprili mwaka huu.
Hii ni kulingana na taarifa kutoka kwa katibu-mkuu wa Umoja huo Ban ki-Moon, iliochapishwa katika mtandao wa mkataba wa Umoja wa Mataifa.
Uwanachama wa ICC utaiwawezesha Palestina kufuatilia mashtaka ya uhalifu wa kivita dhidi ya Israeli katika siku zijazo.
Lakini pia utayawezesha makundi ya wapiganaji wa Kipalestina kushtakiwa.
Palestina
Rais wa Palestina Mahmoud Abass alituma maombi ya kujiunga na mahakama ya uhalifu wa kivita wiki iliyopita, jambo lililoikasirisha Israeli.
Hatua hiyo inajiri huku Marekani na Israel zikipinga hatua hiyo na kusema kuwa itachochea uhasama kati ya Israel na Palestina.
Tayari Israel imesitisha fedha za kila mwezi za Palestina ambazo imekuwa ikichukua kama kodi kwa niaba yake.
Wiki iliopita waziri mkuu nchini Israel Benjamini Netanyahu alisema kuwa hatokubali wanajeshi wake kufikishwa mbele ya mahakama hiyo.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni