Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 18 Desemba 2014

230 WAUAWA NA IS SYRIA


Islamic State
Miili ya Watu zaidi ya 230 wanaoelezwa kuawa na Wanamgambo wa Islamic State imepatikana katika kaburi la pamoja mashariki mwa Syria, Wanaharakati wameeleza.
Rais wa Syria Bashaar Al Assad
Shirika la uangalizi wa haki za binaadam la Syria limesema Watu hao wanakisiwa kuwa jamii ya kabila moja lililokuwa likipambana na kundi la Jihad jimbo la Deir al-Zour.
Kaburi la pamoja liligunduliwa baada ya Watu wa jamii ya kabila la Sheitat kuruhusiwa na Viongozi wa Wanamgambo wa IS kurejea nyumbani.
Mwezi uliopita , Umoja wa Mataifa ulisema umepokea ripoti kuhusu mauaji mjini humo mwezi Agosti.
Wachunguzi wanasema kuwa inaonyesha kuwa mauaji hayo yalitekelezwa na wanamgambo wa Islamic State katika harakati ya kudhibiti rasilimali ya mafuta karibu na Mji wa Mohassan.
Mmoja kati ya manusura amesema aliona vichwa vingi vikiwa vimening'inizwa kwenye kuta, lakini yeye alifanikiwa kutoroka na familia yake.
Mauaji yanaripotiwa kutokea baada ya mazungumzo kati ya pande hizo mbili kuvunjika huku jamii ya kabila la Sheitat ikikataa kutekeleza yale waliyokubaliana na IS.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni