Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 19 Desemba 2014

MASHARTI YA WIMBO WA TAIFA WA CHINA


Bendera ya China
Wimbo wa taifa wa China hautaruhusiwa kuchezwa tena maharusini , matangani, au kwenye hafla zozote zisizo za kiserikali.
Serikali imesema kuwa wimbo wa taifa utaruhusiwa tu kuchezwa katika baadhi ya hafla za kiheshima na zenye maafisa wakuu wa serikali.
Amri hii imetolewa ili kuhakikisha heshima kwa wimbo wa taifa ambao ni ishara ya uhuru wa taifa pamoja na uzalendo, ustawi , nchi yenye nguvu na watu wenye utaifa. Taarifa hii ni kwa mujibu wa shirika la habari la serikali, Xinhua.
Wimbo huo unaojulikana kama "The March of the Volunteers" unaweza kuchezwa katika sherehe muhimu za serikali au mikutano ya kisiasa , hafla za kidipllomasia au hafla zenye wageni wakuu wa kimataifa.
Wimbo huo pia unaweza kuchezwa wakati wanariadha wa China wakiwa wanavishwa medali zao walizoshinda katika mashindano ya kimataifa.
Watakaovunja sheria hio watakosolewa na kisha kuadhibiwa.
Wimbo huo ulitungwa mwaka 1949 na unajumuisha mistari ya kuwaasa wanjeshi kutoogopa vita licha ya kukabiliwa na maadui.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni