Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 18 Desemba 2014

M'MAREKANI AHUSISHWA NA FEDHA BANDIA UG.




Fedha bandia.Raia mmoja wa marekani amehusishwa na utengenezaji fedha bandia nchini Uganda.
Mamlaka ya Marekani imemkamata raia mmoja wa taifa hilo kwa kuongoza kashfa ya kimataifa ya fedha bandia,BBC imebaini.
Ryan Gustafson mwenye umri wa miaka 27 alishtakiwa kwa njama ya kuwa na fedha bandia nje ya Marekani baada ya fedha hizo kutumika katika biashara tofauti za Marekani.
Shirika la kijasusi la Marekani lilifuatilia fedha hizo hadi Kampala ,ambapo walibaini kuna njama ya fedha hizo bandia inayotengeza yuro,rupee pamoja na fedha tofauti za nchi za Afrika.
Mshukiwa huyo anakabiliwa na kifungo cha miaka 25 gerezani.
 Fedha bandia
Maajenti wa FBI waligundua fedha hizo zinatumwa kutoka Uganda.
Alama ya kidole kutoka kwa kifurushi cha fedha hizo ilitoa maelezo ya fedha hizo kutoka kwa bwana Gustafson,raia wa Marekani.
Shirika hilo la maafisa wa ujasusi lilishirikiana na mamlaka ya Uganda ili kuanzisha uchunguzi wa siri kwa lengo la kununua fedha hizo kutoka kwa mshukiwa huyo.
Alikamatwa ,na msako kufanywa katika nyumba yake ambapo fedha bandia za Uganda,Francs za Congo,Cedis za Ghana,Rupees za India na Yuros pamoja na vifaa vya kutengeza fedha bandia.
Mamlaka ya Marekani inakisia kwamba washukiwa hao waliingiza takriban dola millioni 2 fedha bandia katika soko.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni