Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 18 Desemba 2014

ULAYA YAUNGANA ZAIDI DHIDI YA URUSI


Rais wa Baraza la Ulaya,Donald Tusk
Viongozi wa Ulaya wamemaliza kikao chao mjini Brussels Ubelgiji, wakisema kwa sasa wameunga zaidi kuliko ilivyokuwa katika kuikabili Urusi. Viongozi hao wameonyesha kuwa vikwazo vya kiuchumi havitadhoofishwa licha ya matatizo ya kifedha yanayoikabili Urusi. Badala yake hatua mpya za Umoja wa Ulaya zilizokuwa zimewekwa kufuatia Urusi kulitwaa kimabavu jimbo la Crimea zimepitishwa na zitaanza kutumika mwishoni mwa wiki hii
Rais mpya wa Baraza la Ulaya, Donald Tusk akifunga kikao cha viongozi wa EU amesema Urusi na vitendo vyake ni tatizo kubwa la kimkakati linaloikabili Ulaya.
Bwana Tusk, waziri mkuu wa zamani wa Poland, aliongoza kikao cha wakuu wa karibu nchi zote ishirini na nane za Umoja wa Ulaya. Amesema vitendo vya Urusi ndani ya Ukraine na katika Ulaya ni changamoto na alibaini kwamba mataifa ya Umoja wa Ulaya yameungana zaidi kuliko ilivyowahi kuwa huko nyuma katika kukabiliana na Urusi.
Kwa hiyo Bwana Tusk ameonya kuwa Ulaya inahitaji mkakati wa muda mrefu wa aina yake,ambao si tu utakaoshughulikia matatizo katika wiki zijazo na miezi, bali miaka. Wakati huo huo viongozi wamekubaliana vikwazo vipya vinavyopiga marufuku uwekezaji katika jimbo la Crimea, ishara kwamba vikwazo hivyo havitalegezwa hadi Urusi itakapobadili msimamo wake kuhusu jimbo hilo.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni