Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 18 Desemba 2014

WAKURD WAWAKABILI IS MLIMA SINJAR


Wapiganaji wa Kurdi
Wapiganaji wa Kikurdi wamesema wamepeleka kikosi Kaskazini mwa Iraq ili kupambana na wapiganaji wa kundi la Islamic State IS.
Kikosi cha Wakurd 8000 kilianzisha mashambulizi endelevu kuvunja zuio katika mlima Sinjar ili kuwakomboa maelfu ya Wayazidi na watu wengine ambao wamezuiwa huko na kundi la Islamic State.
Operesheni hiyo imeanza jumatano wiki hii kwa ushirikiano na vikosi vya Marekani na wafuasi wanaunga mkono harakati hizo.
Jumla ya mashambulio 50 ya anga yamefanyika katika eneo hilo dhidi ya vikosi vya IS.
Mwandishi wa BBC aliyepo katika eneo hilo anasema wapiganaji wa Kikurdi wametumia nguvu kubwa ili kuhakikisha wanasonga mbele katika operesheni hiyo
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni