Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 28 Februari 2015

MAREKANI KUFUNGUA UBALOZI WAKE CUBA.

 
 Rais Obama
Marekani inasema kuwa itafungua ubalozi wake nchini Cuba kuanzia mwezi Aprili.
Baada ya duru ya pili ya mazungumzo mjini Washington yenye lengo la kurejesha uhusiano kati yao mwanadiplomasia wa cheo cha juu wa Marekani katika nchi za Marekani ya kusini Roberta Jacobson, alisema kuwa itawezekana kufunguliwa kwa ubalozi kabla ya mkutano wa kimaeneo ambao utafanyika nchini Panama kuanzia tarehe kumi mwezi Aprili.
Mkuu wa ujumbe wa Cuba Josefina Vidal alisisitiza kuwa Marekani ni lazima iondoe Cuba kutoka kwa orodha ya nchi ambazo zinaunga mkono Ugaidi kabla ya kurejesha tena uhusiano huo.
Mwezi Disemba Cuba na Marekani walitangaza kuwa walikubaliana kuboresha uhusiano wao baada ya zaidi ya miaka 50 .
chanzo bbc.

UTAFITI;WANAWAKE HUWA NA MPANGO MBADALA.

 
 Wapenzi wawili
Nusu ya wanawake huwa na mpango mbadala ama wa kando ambao wanaweza kukimbilia iwapo uhusiano wao utaharibika.
Utafiti uliofanywa miongoni mwa wanawake 1000 uligundua kuwa asilimia kubwa imeweza kuwaweka wanaume mbadala pindi tu uhusiano walionao unapoharibika.
Cha kushangaza ni kwamba wanawake waliomo katika ndoa huwa na mpango mbadala ikilinganishwa na wale walio katika uhusiano wa kawaida.
Pia imebainika kuwa mpango huo wa kando huenda akawa rafiki wa zamani ambaye amekuwa akimpenda mwanamke huyo.
Wengine huwa wapenzi wa zamani ama hata mume waliyeachana naye,rafiki ama mtu ambaye walikutana katika eneo la mazoezi.
Utafiti huo ulifanywa na kampuni ya utafiti wa mtandaoni wa Onepoll
chanzo bbc.

RINDA LA LUPITA LAPATIKANA.

 
 Mwanafilamu aia wa Knya Lupita Nyong'o akiwa amevaa rinda lililodaiwa kuibwa na baadaye kuridishwa katika chumba chake cha hoteli mjini London
Polisi katika jimbo la Los Angeles nchini Marekani wanasema kuwa wamepata nguo wanayoamini iliibwa kutoka kwa chumba cha hoteli cha mwanafilamu raia wa Kenya Lupita Nyongo baada ya kuvaa nguo hiyo wakati wa sherehe za Oscars.
Maafisa hao wa polisi wanasema walipokea habari hizo kutoka kwa mtandao wa watu maarufu TMZ.
Mtandao huo ulipokea simu kutoka kwa mtu aliyedai kuwa alikuwa ameichukua nguo hiyo kabla ya kuirejesha tena hotelini alipogundua kuwa lulu 6,000 ilizokuwa nazo zilikuwa bandia.
Awali nguo hiyo ilikuwa ikidaiwa kuwa na thamani ya dola 150,000.
chanzo bbc.

WANAOLALA SANA KUSHIKWA NA KIARUSI.


Mgonjwa anayeugua ugonjwa wa kiharusi 
Watu wanaolala kwa zaidi ya masaa manane kwa siku wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa kiharusi,utafiti umesema lakini wataalam hawajua sababu yake.
Utafiti uliofanywa kwa takriban watu 10,000 katika chuo kikuu cha Cambridge ulibaini kwamba wale wanaolala kwa takriban saa nane wana uwezekano mkubwa wa asilimia 46 kupata kiharusi.
Watu wazima hupendelea kulala kati ya saa sita na tisa ili kupumzika vizuri,lakini kulala zaidi hushirikishwa na matatizo ya afya kama vile ugonjwa wa sukari pamoja na ule wa kunenepa kupitia kiasi.
Hatahivyo haijabainika kutoka kwa utafiti huo iwapo kulala kwa zaidi ya saa nane huenda ndiko kunakosababisha matatizo hayo ambayo husababisha kiharusi ama iwapo ni miongoni mwa sababu za magonjwa yasiojulikana.
Utafiti huo ulifanywa miongoni mwa watu walioko na kati ya miaka 42 na 81.
 
Kitengo cha ugonjwa kiharusi
Watafiti walichunguza mienendo yao ya kulala kwa kipindi cha miaka 10 ambapo watu 346 walipatwa na kiharusi.
Baada ya kuangazia athari kama vile miaka na jinsia, watu waliosema wamekuwa wakilala kwa zaidi ya masaa manane walipatikana na hatari ya asilimia 46 kupatwa na ugonjwa huo.
Wale walioweza kulala kwa chini ya masaa sita walipatikana na hatari ya asilimia 18
chanzo bbc

MBUNGE JOHN KOMBA AFARIKI DUNIA.

 
Mbunge wa Mbinga Magharibi Mh. Kapteni John Komba amefariki Dunia leo saa 10 jioni katika Hosptali ya TMJ Mikocheni.
Kwa Mujibu wa mtoto wa Marehemu Bw. Jerry Komba amesema kifo cha marehemu baba yake kimetokana na ugonjwa wa kisukari ambapo amedai kuwa sukari ilishuka ghafla akiwa nyumbani kwake Mbezi Beach Dar es salaam.
"Ni kweli mzee amefariki dakika 50 zilizopita, alikuwa nyumbani amekaa lakini sukari ilishuka ghafla na baadaye kidogo alifariki" amesema Jerry Komba mtoto wa marehemu.
Katibu wa mbunge huyo Bwana Gasper Tumaini amesema kuwa mbunge huyo alikimbizwa katika hospitali ya TMJ ambapo ndipo mauti yamemkuta.
Aidha Bwana Gaspaer Tumaini ameongeza kuwa mwili wa marehemu umehamishiwa katika hosptali ya Lugalo jijini
Dar es salaam ambapo ratiba ya Mazishi bado haijafahamika.
Eatv imewatafuta Afisa habari wa Ofisi ya Bunge ndugu Owen Mwandumbya, Mkurugenzi wa Mambo ya nje na Elimu kwa umma bwana Jesse Mwakasyuka na katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashilila bila mafanikio kwa kuwa hawakupokea simu
chanzo 5eatv.

JESHI LA CHINA LAINGIA SUDANI KUSINI.

 
Wanajeshi wa Uchina waingia Sudan kusini kuweka amani 
Uchina imesema kuwa kikosi chake kwa kwanza maalum cha kijeshi kilichojumuishwa wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa mataifa kimeanza shughuli zake nchini Sudan kusini.
Katika kipindi cha majuma machache yajayo, jumla ya wachina mia saba watawasili nchini humo .
Watakuwa na ndege zisizokua na rubani, vifaru na makombora.
Uchina haijawahi kuwatuma maelfu ya walinda amani , lakini imekuwa zaidi ikitoa misaada kwa ajili ya amani.
chanzo bbc..

KIONGOZI WA UPINZANI AUAWA URUSI.

 
Maafisa wa polisi wakiweka usalama katika eneo ambalo kiongozi wa upinzani nchini Urusi Boris Nemtsov aliuawa 
Mmoja wa wanasiasa maarufu wa upinzani nchini Urusi Boris Nemtsov ameuawa kwa kupigwa risasi kwenye mji mkuu wa nchi hiyo Moscow.
Mwanasiasa huyo alipigwa risasi nne kutoka nyuma na watu waliokuwa ndani ya gari alipokuwa akitembea nje ya makao makuu ya serikali.
Bwana Nemtsov ambaye alihudumu kama naibu waziri mkuu wakati wa uongozi wa rais Boris Yeltsin alikuwa akimshutumu vikali rais Vladimir Putin.
 
Boris Nemtsov
Alikuwa akipanga mkutano ambao ungefanyika kesho Jumapili kupinga kile alichokitaja kuwa vita vinavyoendeshwa na Urusi nchini Ukrain.
Kwenye mahojiano mapema mwezi huu bwana Nemtsov alisema kuwa alikuwa na hofu kuwa rais Putin angemuua.
CHANZO  BBC.

MAFURIKO YAWAUWA WATU 14,MADAGASCAR.

Mafuriko nchini Madagascar yamewaua watu 14 
Watu 14 wameuawa kwenye mafuriko nchini Madagascar ambapo pia wengine 20,000 wamelazimika kuhama makwao.
Mafuriko hayo yaliukumba mji mkuu Antananarivo na maeneo yaliyo karibu.
Utawala unasema kuwa mvua nyingi siku zijazo huenda ikasababisha madhara zaidi.
Mvua kubwa imenyesha nchini humo kwa takriban wiki mbili.
Mwezi uliopita kimbunga Chedza kiliwaua watu 80 nchini Madagascar.
chanzo bbc.

Alhamisi, 26 Februari 2015

BENSOUDA AWASILI UGANDA ,KUNANI

 
 Mwendesha mashtaka mkuu katika mahakama ya ICC Fatou Bensouda
Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC Fatou Bensouda amewasili nchini Uganda ili kutafuta ushahidi kuhusu kesi ya aliyekuwa kamanda mkuu wa wapiganaji wa LRA nchini Uganda .
Dominic Ongwen ambaye alisema alitekwanyara na LRA akiwa mtoto alifikishwa mbele ya mahakama ya ICC mjini Hague mnamo mwezi Januari akikabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kivita.
Mwandishi wa BBC mjini Kamapala anasema kuwa Bensouda atazuru kazkazini mwa Uganda katika ziara ya siku tano ili kuzungumza na mashahidi mbali na kutembelea maeneo yaliotekelezewa uhalifu huo.
Pia anatarajiwa kukutana na rais Yoweri Museveni wa Uganda ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa mahakama hiyo ya ICC akiishtumu kwa kuwabagua viongozi wa Afrika.
chanzo bbc

CHINJA CHINJA WA ISAKAMATWE; NDUGU

Mauaji ya kundi la Islamic State
Dragana Haines mke wa David Haines,mamlaka zinapaswa kumsaka na kumkamata akiwa hai mtu aliyemuua mume wake kwa kumchinja baada ya kutekwa na kundi la wapiganaji wa dola ya kiislam Islamic State wakati akifanya kazi na shirika la misaada la Uingereza.Mtu aliyemchinja David Haines na wengine tayari amefahamika kuwa ni Mohamed Emwazi.
Bi.Dragana amesema tangu alipojua kuwa mmewe David amechinjwa alijipa matumaini moyoni mwake kuwa ipo siku muuaji huyo atafahamika na hatimaye kukamatwa.Lakini baada ya kupatika kwa taarifa hizi za muuaji huyo anasema kuwa itakuwa faraja ya pekee kwa familia za kila aliyeuawa kinyama na wauaji hao, kwa sababu kama atakutwa amekufa anaona hicho kitakuwa ni kifo cha heshima kwa Mohamed Emwazi, lakini maombi yake ni kwamba kukamatwa akiwa hai na afe baadaye.
Kwa upande wake Barak Barfi ambaye ni msemaji wa familia ya Sotloff iliyopoteza ndugu yao pia, anasema kuwa hawana wasiwasi juu ya kukamatwa kwake muuaji huyo Mohamed Emwazi ama JIHAD JOHN.
"Tuna Imani kubwa sana na nchi ambayo vyombo vyake vya usalama na kiintelijensia vitawakamata watu hawa.Tungependa kwenda kumuangalia muuaji huyu ana kwa ana wakati wa mashtaka yake katika mahakama ya Marekani,na pia kuona akitumikia kifungo chake, katika gereza maalumu ambako ataishi huko pekee yake katika upweke.hiyo ndiyo sheria ya Marekani na hivyo ndivyo nchi yetu inavyoshughulikia matatizo kama haya"amesema Barak.
chanzo bbc

NUKLIA; MSIMAMO WA NETANYAHU WAKOSOLEWA.

 
Waziri wa mambo yanje wa Marekani Joh Kerry 
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry amehoji kuhusu shutuma za Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuhusu msimamo wake kuhusu Mpango wa Nuklia wa Iran.
Netanyahu amekosoa Marekani na nchi nyingine za magharibi kwa kile alichokiita ''kushindwa'' kuizuia Iran kutengeneza silaha za nuklia.
Kerry amekosoa Shutuma za Netanyahu alipokuwa akijibu tamko lililotolewa dhidi ya Marekani na nchi za magharibi kuwa ''zimekubali hali halisi kuwa Iran itakuwa na uwezo wa kutengeneza malighafi za kutengeneza silaha za Nuklia miaka michache ijayo''
Akiwa kwenye mkutano kuhusu maswala ya Nuklia mjini Geneva, Waziri Kerry amewaambia maseneta kuwa Rais Obama aliweka wazi kuwa Sera si kuwa Iran kuwa na Silaha za nuklia hivyo amekosoa kauli ya Netanyahu kuwa haAkiwa kwenye mkutano kuhusu maswala ya Nuklia mjini Geneva, Waziri Kerry amewaambia maseneta kuwa Rais Obama aliweka wazi kuwa Sera si kuwa Iran kuwa na Silaha za nuklia hivyo amekosoa kauli ya Netanyahu kuwa haiko sahihi.
CHANZO BBC.

IKULU YA RAIS YASHAMBULIWA SOMALIA.

 
 Alshabaab
Washukiwa kadhaa na wapiganaji wa Kisomali, wamerusha makombora hadi katika ikulu ya Rais katika mji mku wa Somalia Mogadishu.
Wakuu wa usalama wanasema kuwa mlinzi mmoja ameuawa katika shambulio hilo.
Kundi la wapiganaji wa Al-Shabab limeshambulia mara kadhaa mji huo mkuu kwa mabomu, likijaribu kupindua serikali ya taifa hilo inayoungwa mkono na mataifa mbalimbali duniani.
Ijumaa iliyopita, walipuaji wa kujitolea muhanga waliwaua zaidi ya watu 20 walipolenga mkahawa maarufu mjini Mogadishu Central Hotel ulioko karibu na ikulu ya Rais.
CHANZO BBC.

SAVILE AWADHALILISHA 63,HOSPITAL.

 
 Jimmy Savile, mtangazaji wa zamani wa BBC
Uchunguzi zaidi kuhusu mtangazaji maarufu wa zamani katika vipindi vya BBC, Jimmy Savile umebaini kuwa aliwadhalilisha watu 63 kutoka hospitali ya Stoke Mandeville, nchini Uingereza, lakini malalamiko rasmi yaliyotolewa kutokana na vitendo hivyo yalipuuzwa.
Uchunguzi huo umebaini kuwa sifa ya Savile kama "mpenda ngono" ilikuwa inafahamika miongoni mwa baadhi ya wafanyakazi, lakini tuhuma hizo huenda hazikuwafikia viongozi.
Malalamiko rasmi yaliyotolewa mwaka 1977 na baba wa muathirika yalitakiwa kuripotiwa polisi, imesema ripoti hiyo.
Ripoti nyingine imesema "matendo ya habari ya Savile " ingeweza kutokea tena.
Ripoti ya Stoke Mandeville imesema waathirika, walidhalilishwa kutoka mwaka 1968-92, walikuwa na umri wa kuanzia miaka minane hadi 40.
CHANZO BBC

BANGI NI HALALI WASHINTON DIC.

 
 Mji mkuu wa Marekani Washington DC umehalalisha utumizi wa Bangi
Mji mkuu wa Marekani Washington DC umehalalisha utumizi wa Bangi.
Hatua hii ya Washington inafuatia ile ya jimbo la Colorado, Alaska na Washington state ya kuhalalisha matumizi ya mihadarati kwa starehe.
Mpango huo umekubalika na wananchi wengi katika kura ya maoni iliyopigwa Novemba mwaka jana lakini maafisa nchini
humo wametofautiana na wabunge wa Republican ambao ni wengi bungeni uliosababishwa kusitisha eneo hilo kuidhinisha mbinu za kudhibiti na kutoza kodi mhadarati huo.
Sheria hiyo mpya itaanza kutumika kuanzia saa tano usiku wa Alhamisi na hivyo mtu yeyote atakayekuwa akimiliki bangi kisiri atakuwa huru kuivuta bila hofu ya kukamatwa..
Sheria hiyo mpya hata hivyo imezua tofauti baina ya Meya wa mji huo na bunge la Congress.
Weneyji wa mji huo wenye umri unaozidi miaka 21 watakuwa huru kumiliki gramu 56 ya Bangi.
 
Meya wa Washington Muriel Bowser
Aidha wanauwezo wa kuipanda majumbani mwao.
Hata hivyo sheria hiyo mpya inaharamisha kuuzwa kwa bangi na ununuzi wake.
Mji mkuu wa Washington DC - ni wilaya maalum lakini haina uhuru na hadhi sawa na majimbo kwa hivyo kuna dhana kuwa ilikiuka kanuni ilipoamua kupiga kura ya maoni.
Katika Barua iliyoandikwa na wajumbe wa bunge hilo la Congress,Meya wa Washington Muriel Bowser ameonywa kuwa sheria za jimbo zinakiukwa iwapo sheria hiyo maarufu itaanza kutekelezwa.
Wajumbe hao wanadai kuwa kulingana na sheria maalum iliyopitishwa na Bajeti ya taifa Kuhalalishwa kwa bangi ni haramu.
Bi Bowser hata hivyo anaendelea kushikilia kukutu kuwa walifwata kanuni zote zilizowekwa.
CHANZO  BBC

MCHINJAJI WA IS 'JIHADI JONH'ATAMBULIWA

 
 Mwanaume ambaye amekuwa akitekeleza mauaji ya mateka wa kundi la wapiganaji wa Islamic State ajulikanaye kwa jina la utani "Jihadi John",ametambuliwa.
Mwanaume ambaye amekuwa akitekeleza mauaji ya mateka wa kundi la wapiganaji wa Islamic State ajulikanaye kwa jina la utani "Jihadi John",ametambuliwa.
Bwana huyo ambaye taswira yake akiwachinja mateka kwa kisu bila huruma ndiyo nembo ya wapiganaji hao sasa ametambuliwa kuwa anatokea Uingereza.
Shirika la Habari la BBC limetambua kuwa jina lake kamili ni Mohammed Emwazi.
Emnuazi ameonekana kwenye video kadhaa ya mauwaji ya mateka wa mataifa wa magharibi, akiwemo Mmarekani James Foley, Raia wa Uingereza, Alan Henning na mwaandishi habari wa Japan, Kenji Goto.
Inaaminika kuwa Emwazi ni raia wa Uingereza na hasa anatokea magharibi mwa London.
Yamkini Emnuazi aliyezaliwa Kuwaiti na mwenye umri wa kati ya miaka 20 -29 alikuwa amefahamika sana na vyombo vya usalama lakini kwa sababu za kiusalama haikuwezekana kumtambua.
Anaaminika amewahi kuishi Somalia mnamo mwaka 2006 na anauhusiano mkubwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabab nchini humo.
Polisi nchini Uingereza imeziomba vyombo vya habari kutosambaza habari ambazo hawajazithibitisha kumhusu jamaa huyo kwani uchunguzi unaendelea.
Hata hivyo bado habari za kina kumhusu Jihadi John hazijatolewa.
Mwandishi wa maswala ya Usalama wa BBC Tomi Oladipo anasema kuwa vyombo vya usalama vya serikali za mataifa yanayokaribia Somalia sasa yana kila sababu ya kutahamaki.
 
Bwana huyo aliwahi kushirikiana na kundi la Al Shaabab
Kwa sababu Kuhusika kwake na kundi la Al Shaabab kisha akajiunga na kundi la Islamic State ambalo kwa wakati mmoja lilikuwa linashindana na wanamgambo wa Al Qaeda kuhusu yupi kati yao anayeushawishi
mkubwa
Ishara kuwa Al Shabab inazingatia msimamo mkali wa kidni hata zaidi ya Al Qaeda.
Kwa sababu itakumbukwa kuwa Al Qaeda ilipinga hatua kali ya kuwachinja mateka nchini Iraq na Syria.
Emnuazi ambaye amekuwa akiwabeza mataifa ya Magharibi kabla ya kuwakata shingo naaminika kuwa mtaalamu wa maswala ya kompyuta alisomea chuo kikuu cha Westminster.
Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC bwana huyo anaaminika kuwa alikwenda Syria mwaka wa 2012, lakini kabla ya wakati huo majasusi wa Uingereza na Marekani walikuwa hawajajua tishio lake.
CHANZO BBC.

NGOMA NA VUVUZELA ZAIPIKU SIMU MALAWI.

Nchini Malawi vuvuzela inaaminika zaidi kuliko simu.
Jamii nchini Malawi wanapendelea zaidi kuwasiliana kwa njia za asili zaidi ya kuliko ambavyo karne hii ya sayansi na teknolojia inavyofanya,hivyo jamii hizo hutumia zaidi ngoma za asili,ama vuvuzela kama njia ya mawasiliano na wamezipa kisogo simu za kisasa ama radio pale ambapo jamii yao ikikumbwa na janga lolote, basi njia za asili ndio mwafaka kwao.
Kwa kawaida sisi hutumia njia hizi za asili kwasababu simu za kisasa haziaminiki,asema bwana Ndamiwe Kalambo,na pia amewataka viongozi wa kiserikali pamoja na wananchi wajadili kwa kina juu ya masuala ya majanga ya asili pindi yatakapo watokea kama mafuriko ni hatua gani ambazo watapaswa kuzichukua na kufikisha taarifa kwa wakati.
Akitetea hoja ya utumizi njia za asili zaidi Ndamiwe anasema kwamba maeneo mengi ya nchi hiyo hayana mawasiliano ya uhakika na hata mtandao haukamati asilani,na hivyo hata ujumbe wa dharura utumwapo haufiki kwa wakati kwa wahusika na hivyo mawasiliano ya kisasa si rahisi hivyo.
 
Chombo hiki malawi sio ssaaaana kiviiile.
Taarifa zinaeleza kwamba jamii ya Kilupula ilikumbwa na mafuriko,kulikuwa na mkutano wanakijiji walikuwa wakipiga mayowe ya kuomba msaada,wengine walikuwa wakipiga ngoma,wengine walikuwa wakipuliza filimbi ama vuvuzela ili kupeleka ujumbe wa dharula ama mwito wa kuomba msaada.
Kalambo aliwaambia viongozi wa kiserikali kuwa ,ujumbe wa serikali wa dharula ama kuomba msaada unapaswa kusambazwa kwa jamii nzima ya Malawi kwa ujumbe mfupi sawa na wakati wa upigaji kura ili kuongeza nafasi ya ujumbe mfupi kuwafikia walengwa kwa wakati.
Tangu mwaka 1984,Malawi imeshakumbwa na mafuriko mara ishirini na tisa,imepigwa na vimbunga mara tatu na imeshakumbwa na ukame mara saba, na njia ya mawasiliano wanayoitumia zaidi ni ya asili na vuvuzela linaongoza kwa matumizi.
Wengine wanalitumia vuvuzela michezoni lakini Malawi wanalitumia kama njia ya mawasiliano.
chanzo bbc.

EBOLA; MFANYAKAZI APOTEZA MAISHA.

Mfanyakazi wa kituo cha yatima Augustine Baker 
Raia mmoja wa Sierra Leone aliyekuwa akiwatunza Watoto walioachwa yatima kutokana na ugonjwa wa Ebola amekufa kutokana na ugonjwa huo.
Augustine Baker alifikishwa katika kituo cha matibabu baada ya kuugua juma lililopita.
Baker alikuwa akifanya kazi katika Kituo cha Watoto yatima kinachoendeshwa na kituo cha msaada kutoka Uingereza.Kituo hicho kiko nje ya mji wa Freetown.
Watoto 33 na Wafanyakazi saba katika nyumba ya yatima St George, wamewekwa katika Karantini tangu Bwana Baker alipobainika kuwa na Virusi vya Ebola.
Kituo hiki kilianzishwa mwaka 2004 mpaka pale Ugonjwa wa Ebola ulipoingia, kituo kilijikita zaidi katika kuwaokoa Watoto wa mitaani.
Mwaka jana kituo kiliwasaidia Watoto takriban 200 walioachwa na familia kutokana na Ebola.
Ebola imeua zaidi ya Watu 9,500 nchini humo,Liberia na Guinea.
Lakini katika kipindi cha majuma ya hivi karibuni, kasi ya maambukizi ya Ugonjwa huu imepungua na Serikali za nchi tatu zimeahidi kumaliza kabisa tatizo hili ndani ya miezi miwili ijayo.
chanzo bbc.

Jumatano, 25 Februari 2015

MAHABA NIUE......


MWANAFUNZI AMUUA MWENZAKE KWA NGUMI SHINYANGA.

 
 Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga kamishina msaidizi Justus Kamugisha.
 Mwanafunzi wa shule ya msingi Ilola kata ya Ilola, Itwangi wilaya ya Shinyanga vijijini mkoani hapa, Sophia Mathew (12), anashikiliwa na polisi kwa kumuua mwenzake wakati wakigombea daftari kwa kumpiga ngumi kichwani na kuangukia kisogo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Longinus Tibishubwamu, amesema tukio hilo limetokea juzi saa 7:30 mchana, wakati wanafunzi hao wakiwania daftari walioazima waliposababisha ugomvi mkubwa.
Tibishubwamu amemtaja mwanafunzi amefariki dunia ni Veronica Venance (12), anayesoma darasa moja na mwenzake aliyesababishia mauaji hayo.
Akizungumza na ea radio leo, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Magere Jonas, amesema wakati wanafunzi hao wanagombea daftari hilo, alikuwa amepumzika chini ya mti akiwa na mwalimu mkuu msaidizi, na ghafla wakaletewa taarifa na wanafunzi wenzao wanagombana darasani.
Jonas amefafanua mara baada ya kuingia darasani wakamkuta mwanafunzi huyo akiwa amelala chini anagalagala, hivyo kuchukua jukumu la kumkimbiza kwenye kituo cha afya Bugisi jirani na shule hiyo lakini kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo alifariki dunia.
Hata hivyo, mtendaji wa kata ya Ilola, Mahona Joseph, amekiri kutokea kwa tukio hilo na kuongeza marehemu alikuwa ameng’anga’nia daftari alilokuwa ameazimwa na Sophia Mathew kwa ajili ya kuandika (notes) kitendo ambacho kilimkera mwenzake huyo na kuzua ugomvi.
Aidha, Kaimu kamanda wa polisi mkoani humo, Tibishubwamu, amesema wanamshikilia mwanafunzi huyo kwa mahojiano zaidi pamoja na kufanya upelelezi juu ya tukio hilo na uchunguzi utakapokamilika watamfikisha mahakamani ili kupewa adhabu inayostahili.
CHANZO 5EATV.

MADONNA AANGUKA KATIKA TUZO ZA BRITS.

 
 Kinara wa tuzo za Brits Ed Sheeran
Tuzo kuu nchini Uingereza za muziki, the Brits, zimetolewa London. Ed Sheeran alichaguliwa kama msanii bora mwanamume wa kipekee Uingereza. Taylor Swift, alitajwa kama msanii mwanamke wa kimataifa wa kipekee. Katika sherehe hizo.
Madonna aanguka katika sherehe hizo
 Mwanamziki Madonna akiwa ameanguka jukwaani katika tuzo za Brits
Hata hivyo muimbaji maarufu, Madonna alikumbwa na mkosi wa aina yake ambao ulimharibia siku baada ya kujikwaa katika ngazi na kuanguka mbele ya kadamnasi.

WAFUASI WATATU WA IS,WAKAMATWA MAREKANI.

 
 Rais wa Marekani Barack Obama
Maafisa wa Polisi nchini Marekani,wamewakamata wanaume watatu kwa njama za kuwaunga mkono wanamgambo wa dola ya kiislam Islamic State.
Wanaume wote hao ni wakaazi wa mji mkuu wa nchi hiyo New York. Wawili kati yao wanatokea Kazakhstan na Uzbekistan, na mwingine ni wa kutoka Uzbek yeye alimakatwa mjini Florida.
Wawili kati ya wanaume hao walikuwa na mpango wa kusafiri kuelekea nchini Syria .
 Wapiganaji wa Islamic State
Kwa mujibu wa Shirika la Ujasusi la Marekani FBI watuhumiwa wawili kati yao walitishia kuwaua maafisa wa polisi kama wasingeweza kusafiri kwenda Syria.
Hata hivyo mtuhumiwa mmoja kati ya watuhumiwa hao alikuwa na mpango wa kumuua rais Marekani Barack Obama,wamesema FBI.
Kamishina wa polisi mjini New York , William Bratton anasema maneno yao ndiyo yanayodhihirisha nia yao.Hata hivyo inadaiwa kuwa ni dhahiri kutokana na matamshi yao walikuwa na mpango wa kusafiri hadi nchini Syria, baada ya kukamilisha malengo yao ya kijipatia silaha ambazo wangezitumia kuwashambulia maofisa wa polisi.
Bratton amesema ilikuwa ni mpango wao wa wazi kwamba hawakuhitaji kwenda,huku malengo yao ikiwa ni kujipatia silaha kama vile bunduki aina ya mashine gani, kwa lengo la mashambulizi maalum dhidi ya maofisa wa polisi ambapo maneno yao ya kuhamasishana yalikuwa wazi kwa mjibu wa maneno yao.
Nje ya mahakama mjini New York walikofikishwa washitakiwa wawili mwanasheria wa washitakiwa hao, Adam Parumata ameelezea kutoridhirishwa na mwenendo wa mashitaka hayo dhidi ya wateja wake.
"Kama tuhuma hizi ni za kweli,na bado ni tuhuma tu, zinatufanya kujiuliza maswali mengi kwa jinsi serikali inavyowachukulia vijana hawa,na watu wa dini ya Kiislam ndani ya Marekani. Kwani wapo katika uangalizi mkali na wa aina yake,hakuna ruksa kujibu,kuzungumza, kudadisi wala kueleweshwa. Kinachofanyika ni mbio mbioni kuwafungulia mashtaka, kuwaweka kizuizini. Nataka kusisitiza jambo kwa kila mtu leo kuwa haki ya mshitakiwa ni kwamjibu wa sheria za Marekani,hivyo tunafanya kila linalowezekana kupigania haki katika kesi hii kwa lengo la kulinda haki”amesema Parumata.
chanzo bbc.

WAETHOPIA 13,WAKAMATWA WAKISAFIRISHWA MOROGORO.

 
 Jeshi la polisi mkoa wa Morogoro limewakamata wahamiaji haramu 13 kutoka nchini Ethiopia wakiwa kwenye gari ndogo aina Prado katika kijiji cha Lusanga Turiani wilayani Mvomero wakijiandaa kwenda Afrika kusini kupitia mkoani Mbeya

JE,KIPOFU HUONA GIZA?

 
 mlemavu wa macho
Mwandishi wa BBC Damon Rose alipofuka alipokuwa mtoto lakini anasema kuwa sio kwamba anaona giza.
Je, yeye anaona nini haswa?.hudhaniwa kwamba watu waliopofuka huona weusi tititi,lakini kulingana na uzoefu wa mwandishi huyu hilo si kweli.
Anasema kwamba kila anapoulizwa ni nini haswa anachokikosa kwa kuwa kipofu yeye husema ni giza.
Anasema kuwa yeye ni mmoja ya watu ambao hawaoni kabisa.
Alipofuka miaka 31 iliopita baada ya kufanyiwa upasuaji ambao haukufaulu.
 Rangi wanazoona watu waliofofuka
Watu hudhania kwamba mwanagaza unapoondolewa basi mtu husalia katika giza.
''Unapoingia katika matandiko huwezi kuona kitu kabisa.Unapofunga macho kila kitu kinabadilika na kuwa giza''.
''Kwa hivyo upofu ni sawa na giza? Inaingia maanani lakini si kweli''.
''Ijapokuwa uhusiano wangu wa akili na macho umekatika duniani haijawa giza kwangu''.
Kwa hivyo unapopofuka ni nini haswa unachoona? aliulizwa mwandishi huyu. ,''jibu ni mwangaza,mwangaza mwingi sana ,rangi za kung'ara,rangi nyingi zinazobadilika kila mara na mwangaza mbaya ulio na bughudha''.

WANAUME WATATU WAOANATHAILAND.

Wanaume watatu waliooana nchini Thailand wapata umaarufu
Wanaume watatu waliofunga ndoa siku ya wapendanao {Valentine} nchini Thailand wamepata umaarufu katika mtandao baada ya picha za maandalizi ya harusi hiyo kuenea mitandaoni.
Watu hao walijulikana kama Joke,Bell na Art ambao walioana saa sita, usiku wa tarehe 15 mwezi Februari mwaka huu.
Kulingana na gazeti picha hizo zinawaonyesha wanandoa hao watatu wakiwa wamevalia nguo za utamaduni wa Thai uliochanganyika na utamaduni wa magharibi.
Ujumbe mmoja ulioandikwa katika katika picha moja ulisoma' mapenzi ya kweli hayawezi kuonekana na macho pekee'.
''Iwapo unataka kujua thamani yako basi ni lazima uione na moyo wako''.
katika mtandao wa facebook wa runinga moja ,picha ya wanandoa hao ilipendwa na zaidi ya watu 50,000 huku watu 1000 wakitoa maoni yao.
CHANZO BBC.

DAWA YA KUPAKA ILI KUZUIA HIV HAIFAI.

Dawa za ugonjwa wa ukimwi 
Dawa iliokisiwa kupunguza uwezekano wa mwanamke kupata virusi vya HIV wakati wa tendo la ngono haifai,kulingana na utafiti mkubwa uliofanywa na shirika la Follow on Africa Consortium for Tenofovir kutoka Afrika kusini.
Matokeo ya utafiti huo unaojulikana kama facts 001 yalitolewa katika kongamano la magonjwa ya virusi na yale ya maambukizi nchini Marekani.
Kulingana na gazeti la mail and Guardian nchini Afrika kusini,wanawake katika utafti huo waliagizwa kujipaka dawa hiyo katika sehemu zao za siri kabla na kila baada ya tendo la ngono.
Matokeo hayo yanapinga matokeo ya utafiti mwengine uliochapishwa mwaka 2010 na shirika la mpango wa utafiti wa ugonjwa wa ukimwi nchini Afrika kusini Caprisa.
Watafiti waliwatumia zaidi ya wanawake 900 katika jimbo la Kwa Zulu Natal na kuripoti dawa hiyo ya Tenofivir ilikuwa na uwezo wa asilimia 39 pekee wa kupunguza viwango vya maambukizi ya viini vya HIV miongoni mwa wanawake hao.
Viwango vya maambukizi ya HIV nchini Afrika kusini vilikuwa asilimia 12.2 mwaka 2012 ikiwa ni vya juu zaidi duniani kulingana na utafiti wa baraza la sayansi ya binaadamu kuhusu kinga ya HIV ,visa na tabia.
Viwango hiyo ni vya juu miongoni mwa wanawake na kusababisha utafiti kutafuta tiba za kinga zinazowalenga wanawake kama vile dawa inayopakwa katika sehemu za siri,pamoja na sindano zilizojaa tiba za kukabiliana na HIV.
Wakati wa utafiti huo uliochukua takriban miaka mitatu,watafiti waliwatumia wanawake 2000 wasio na virusi vya ukimwi kati ya miaka 18 hadi 30, na kuwapatia nusu yao dawa ya Placebo na nusu nyengine wakapewa dawa ya kwenye sehemu za siri tenofivir,ambayo ni dawa ya kukabiliana na virusi vya ukimwi.
Baadaye watafiti walipima viwango vya maabumizi ya virusi vya HIV kati ya makundi mawili na kubaini kwamba wanawake waliopewa dawa hiyo ya Tenofivir waliambukizwa virusi vya ukimwi sambamba na wanawake waliopewa dawa kupaka ya placebo.
Kwa jumla wanawake 123 waliambukizwa virusi vya HIV huku 61 wakiwa ni wale waliopewa mafuta ya Tenofivir na 62 wakiwa walipewa mafuta ya placebo.
CHANZO BBC.

UANDIKISHAJI KWA E;EKTRONIK UMESHINDWA ?

Teknolojia mpya inaelezwa kukumbwa na changamoto inayokwamisha zoezi la uandikishaji kufanyika kwa ufanisi
Vyama vya upinzani nchini Tanzania vimeendelea kuishinikiza serikali kuachana na mpango wa kura ya maoni juu ya katiba inayopendekezwa na badala yake itatue changamoto zinazojitokeza wakati wa kuandika wapiga kura kwa kutumia mitambo ya BVR ili iweze kukamilika kwa ufanisi.
CHADEMA, CUF, NCCR MAGEUZI na NLD kupitia uongozi wao vimesema serikali inatakiwa kusikiliza malalamiko yanayotolewa juu ya namna mfumo wa uandikishaji unaoendelea ili kazi hiyo isikwamishe uchaguzi uchaguzi mkuu.
Moja ya changamoto zinazozungumziwa ni pamoja na idadi ndogo ya mashine hizo kuweza kumudu idadi ya wale wanaotakiwa kuandikishwa.
Awali, mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi alieleza BBC kuwa mpaka zoezi linaanza zilikuwepo mashine 250 tu kati ya 8000 zinazohitajika lakini akadai 7,750 zilizosalia serikali ilikuwa imeshazilipia na zinategemewa kufika nchini wiki ya kwanza ya mwezi wa tatu.
"Habari tulizo nazo siyo hata mashine zote zinafanya kazi hi sasa huko Njombe, bali ni mashine 82 tu huku nyingine zikiwa zimepelekwa kufundishia watakaoandikisha katika mikoa mingine" Amesema Freeman Mbowe Mwenyekiti wa chama kiii cha upinzani CHADEMA.
Vile vile kutokana na mashine hizo kuwa na sehemu iliyotengenezwa na bati katika eneo lake la chini zilikuwa zinapata joto, hata hivyoTume inasema changamoto hiyo imetatuliwa.
Kasoro nyingine iliyojitokeza ni mashine hizo kushindwa kutambua alama za vidole vya baadhi ya watu ambao ngozi zao za vidole zina michubuko.
Aidha, mashine hizo zimekuwa zikitumia muda mwingi kuhifadhi taarifa za mtu mmoja jambo ambalo linaleta hofu iwapo kazi hiyo itakamilika mapema na kwa ufanisi.
Lengo la kuandika wapiga kura kwa njia ya mitambo ya BVR ni kuboresha daftari la wapiga kura ambalo lilikuwa linalalamikiwa na vyama vya siasa kuwa lina upungufu mwingi ikiwamo uwezekano wa kumruhusu mtu kupiga kura zaidi ya mara moja.
Iwapo kazi hii itakamilika, kumbukumbuku zitakazohifadhiwa na mitambo hiyo zitatumika mwezi aprili wakati wa kupiga kura ya maoni ya kuamua iwapo Katiba mpya inayopendekezwa inafaa au la na baadae katika uchaguzi mkuu uanaotarajiwa mwezi oktoba mwaka huu.

WAISALAMU TAABANI AUSTRIA KUNANI??

 
 Bunge la Austria lajiandaa kujadili mswada utakaowanyima waislamu uhuru wa kupokea msaada wa kimataifa
Bunge la Austria linajiandaa kujadili mabadiliko yenye utata kuhusiana na sheria dhidi ya Uislamu.
Sheria hiyo mpya itazuia ufadhili wa kifedha kutoka mataifa ya nje katika ujenzi wa misikiti .
Ufufuaji wa sheria hiyo iliyodumu nchini humo kwa kipindi cha karne moja iliyopita utawaruhusu wakristu na wayahudi kupata ufadhili kutoka mataifa ya kigeni ilahali inawanyima waislamu uhuru wa kupokea msaada kutoka
ughaibuni.
 Wakristu na wayahudi wataruhusiwa kupokea misaada iwapo sheria hiyo itapitishwa lakini Waislamu na Masheikh hawatoruhusiwa
Kwa mujibu wa waziri wa mtagusano na umoja wa taifa, Sebastian Kurz, sheria hiyo inalenga kuilinda mtagusano wa taifa japo viongozi wa Kiislamu wamepinga vikali mswada huo wakisema utawabagua.
Bwana Kurz amesema wazo la kubadilisha sheria hiyo limetokana na mashambulizi yaliyotokea huko Ufaransa na Denmark.
Aidha mapumziko ya siku zao takatifu kutoka kazini bila ya kupewa adhabu na pia kupata muongozo wa kiroho katika taasisi kadha za serikali kama vile magereza na hospitalini.
CHANZO BBC.

WAETHIOPIA 100 WAHUKUMIWA KUWA KENYA.

 
 Raia mia moja wa Ethiopia hii leo wamehukumiwa kifungo cha miezi kumi na mbili gerezani nchini Kenya au walipe faini ya takriban dola 600
Raia mia moja wa Ethiopia hii leo wamehukumiwa kifungo cha miezi kumi na mbili gerezani nchini Kenya au walipe faini ya takriban dola 600 baada ya kupatikana na hatia ya kuwemo Kenya kinyume na sheria.
Polisi waliwakamata wahamiaji wao haramu siku ya Jumatatu katika mtaa mmoja mjini Nairobi. Maryam Dodo Abdalla anaarifu zaidi.
Wahamiaji hao haramu walioonekana wachafu na waliodhoofika kwa njaa, walikiri mashtaka hayo baada ya kusomewa makosa yao mmoja baada ya mwingine na hakimu Victor Wakhumile mjini Nairobi.
Sasa wanatakiwa kutumikia kifungo hicho au walipe faini waliotozwa, na baadaye watasafirishwa kurudishwa Ethiopia walikotoka.
Kwa kilio, wameielezea mahakama kwamba wamewasili Kenya wakiwa wanaelekea Afrika kusini ambako wameahidiwa kupewa ajira.
Polisi nchini kenya iliwanasa raia hao mia moja wa Ethiopia, mapema wiki hii wakiwa wamehifadhiwa katika chumba kimoja kidogo, eneo la Embakasi mjini Nairobi.
Mkuu wa kitengo maalum cha kuzuia uhalifu nchini, SCPU, Noah Katumo amesema kwamba waliwakamata baada ya kupata fununu kwamba kuna wageni wengi waliowasili katika mabasi mawili tofuati kutoka Ethiopia katika mtaa huo.
Raia mia moja wa Ethiopia hii leo wamehukumiwa kifungo cha miezi kumi na mbili gerezani nchini Kenya au walipe faini ya takriban dola 600
Miezi kadhaa ya nyuma, wahamiaji wengine zaidi ya mia moja kutoka Ethiopia walihukumiwa kwa makosa kama hayo ya kuwepo Kenya kinyume cha sheria na walihukumiwa miezi sita gerezani.
Ni wahamiaji wengi haramu wanaovuka mpaka na kuingia Kenya kutoka Ethiopia.
Wengi huitumia Kenya miongoni mwa nchi nyengine kama pia Tanzania, Msumbiji Malawi na Zambia kama njia ya kupita kuelekea Afrika kusini.
Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kimataifa la wahamiaji, IOM, ni wahamiaji 17,000 hadi 20,000 wanaoelekea Afrika kusini kila mwaka.
Asilimia 60 ya idadi hii ni wanaume kutoka Ethiopia wanaohadaiwa kwamba watapata ajira na maisha mazuri.
Katika mahakama hiyo hiyo leo, raia watatu wa Kenya wameshtakiwa kwa makosa ya kuwasafirisha kiharamu raia hao 100 wa Ethiopia.
Hatahivyo wamekana mashtaka na kuachiliwa kwa dhamana ya takriban dola 950 na kesi yao sasa inatarajiwa kutajwa tena tarehe 11 mwezi Machi.
CHANZO BBC.

WAKRISTO ZAIDI WATEKWA NYARA SYRIA.

 
 Kuna hofu kuwa raia wakristo kutoka Syria wametekwa nyara na wanamgambo wa Islamic State.
Kuna hofu kuwa raia wakristo kutoka Syria wametekwa nyara na wanamgambo wa Islamic State.
Duru kutoka kwa jamii hiyo sasa inathibitisha kwamba zaidi ya raia 200 walitekwa nyara Jumanne baada ya vijiji kadhaa kushambuliwa kazkazini mwa Syria.
Wengi wa waliotekwa nyara ni wanawake na wazee.
Wakati huo huo, mapigano yangali yakiendelea katika maeneo yaliyoko karibu na mji wa Hassaka.
Kuna taarifa zinazosema kuwa makanisa yameteketezwa moto na kundi la IS katika vita hivyo vikali kati ya wanamgambo hao na makabila ya Wakurdi wanaoungwa mkono na wakristo wenye silaha.
Taswira kamili ya mkasa uliowakumba wakristu hawa wa Syria ndio mwanzo unaanza kujitokeza.
 Wakristo kutoka Syria wameanza kutoroka wanakoishi
Lakini kikundi cha wapiganaji wa kikristu kimetoa madai kuwa idadi hiyo ni kubwa hata zaidi ya hiyo.
Kimedokeza kuwa zaidi ya watu mia tatu hamsini wametekwa.
Huku hayo yakiarifiwa waumii wengine wa kikristu wameanza kukimbia avijiji vyao wakihofia kushambuliwa na wanamgambo wa Islamic State.
Na bado vita vinaendelea huku waislamu hao wakikabiliana na waasi wa kikurdi pamoja na washirika wao wa kiksristu katika mji wa Hassaka.
CHANO BBC.

Jumanne, 24 Februari 2015

ALIYEWALAWITI WATOTO KENYA KUHUKUMIWA

 Raia wa Uingereza aliyewadhalilisha kingono watoto wa kiume katika mji mdogo wa Gilgil nchini Kenya anatarajiwa kuhukumiwa leo nchini Uingereza.
Hii ni baada ya Mahakama ya Birmingham kumkuta na hatia ya kuwadhalilisha watoto wa kiume kingono na pia kupatikana na picha za utupu za watoto.
Simon Harris mwenye umri wa miaka 55 ambaye alikuwa akiendesha Mradi wa misaada kwa Jamii anaaminika kufanya maovu hayo kwa karibu miaka ishirini.
Gladys Njoroge amekutana na baadhi ya waathirika ambao waliomba majina yao yahifadhiwe.
CHANZO BBC.

KOMBE LA DUNIA NI NOVEMBA NA DECEMBER.

 
 Qatar na Urusi kuwa wenyeji wa kombe la dunia mwaka 2018 na 2022 ilijulikana miaka nane iliyopita.
Wakuu wa mpira wa miguu wamekutana mjini Doha kujadili juu ya masuala kadhaa ya kuchagua juu ya hali ya majira ya kiangazi endapo yataathiri afya ya wanamichezo na mashabiki wao.
Majira ya kiangazi nchini Qatar hakizidi nyuzi joto 40C na mwezi wa November na mwezi December hushuka na kufikia nyuzi joto 25.
Kikosi kazi hicho kinaongozwa na chief Sheikh Salman bin Ebrahim Al-Khalifa na amesema kwamba michuano hiyo ya kombe la dunia ya mwaka 2022 inapaswa kupigwa kwa siku chache tu .
Pamoja na mipango na kauli mbalimbali tayari kuna utabiri unaoonesha kuwa michuano hiyo inaweza kuanz arasmi mnamo tarehe 26 November na kwisha tarehe 23 December.
Hata hivyo, Fifa imesema haina mpango wa kupunguza muda wa michuano hiyo kutoka timu 32 ama michezo 64 .
 Qatar na Urusi walijulikana miaka minne iliyopita kuwa wenyeji wa michuano hiyo
Kwanini November-December?
Fifa imesema kwamba imeshafanya uchaguzi wa namna mbali mbali katika masuala mengi na kujadili pia lakini imeona kwamba miezi hiyo November-December ni bora zaidi na sababu za fifa ni hizi katika kutetea hoja yake .
Miezi ya January-February micguano hiyo itakwaana na michuano ya majira ya baridi ya OlympicsMwezi wan ne ni mwezi mtukufu wa Ramadhani ambao unatarajiwa mfungo kuanza tarehe 2 April mwaka 2022Hali ya joto inatarajiwa kudumu kutoka mwezi May hadi September nchini Qatar
Katibu mkuu wa Fifa Jerome Valcke kumekuwa na faida na hasara ya chaguo lakini suluhisho ni miezi hiyo ya November na December.
Sheikh Salman anasema wameridhishwa, nah ii ni baada ya uzingatifu makini wa mawazo tofauti tofauti na majadiliano ya kina na wadau wa soka ,tumetambua kile tunachokitaka na ndio suluhisho la michuano ya kimataifa ya mwaka 2018-2024 na kandanda kwa ujumla wake .
 
Nyasi zitachakazwa
Juu ya fainali kuwa 23 December?

WASHIKAJI BUNDUKI WAMUACHA BROOKLYN.

 
Brooklyn wa mbele 
Brooklyn Beckham,ambaye ni mtoto wa mwanasoka na nahodha wa zamani wa timu ya England, amebaki njia panda baada ya jaribio lake la kutaka kutetea udhamini wake na timu ya Arsenal .
Brooklyn mwenye umri wa miaka 15, alikuwa akijihusisha na chuo cha timu hiyo cha Hale End academy na alikuwa na matumaini ya kupata mkataba wa miaka miwili kuendelea na washika bunduki hao.
Hata hivyo, imeelezwa kuwa kijana huyo hatakuwa chuoni hapo msimu ujao na hapo ndio atakuwa amemaliza mkataba wake na Arsenal.
Taarifa hii imekuja bila kutegemewa baada ya baba wa kijana huyo kupigiwa simu na klabu hiyo ya vijana walio chini ya miaka 18 mapema mwezi huu .
Imetanabahishwa kuwa kijana huyo wa Beckham alikuwa pekee kati ya walio na umri wa chini ya miaka 16 na chini ya miaka 17 kusalia klabuni hapo Hale End academy wakati wengine wote Al Kass kwenye michuano ya vijana huko Qatar.
Beckham atasalia kwenye klabu hiyo mpaka mwishoni mwa msimu na haijafahamika mara moja kama kijana huyo atatafuta klabu nyingine ya kuelekea.
Pamoja na uamuzi wa kutomsajili kijana huyo katika klabu ya Arsenal kocha wa vijana chipkizi bado anamhesabu kijana huyo kuwa na kipaji cha hali ya juu lakini wapo vijana wengine ambao wanamzidi kwa mbali katika safu ya kiungo ambayo ni ya juu klabuni hapo. Na wanamuona Brooklyn kuwa anaweza kucheza vizuri zaidi akiwa na klabu nyingine akiamua .
Watoto wengine wa Beckham Romeo na Cruz wako katika chuo hicho cha Hale End. Cruz, mwenye miaka 10, naye anakuja juu zaidi ya nduguze kwenye soka na ameelezwa kuwa ana kipaji cha hali ya juu.
CHANZO BBC.

JE,UNASIMU YA ANDROID ?SOMA HAPA ?.

 
 Utafiti umebaini kuwa betri za simu za android zinawezakutumika kufuatilia watumizi
Simu za kisasa zinazotumia mfumo wa Android zinaweza kufuatiliwa kwa urahisi sana.
Uchnguzi umebaini kuwa simu zinazotumia mfumo huo zinaweza kufuatiliwa kwa urahisi mno pasi na kutumia kifaa cha GPS yake.
Aidha simu hizo zinaweza kudukuliwa kwa kutumia matumizi ya betri yake huku utafiti ukisema kuwa simu zinazotumika karibu na kifaa cha kupeperushia masafa ya simu za kuungia mbali.
Simu za kisasa ''Smartphone'' hutumia nguvu zaidi inapokuwa mbali zaidi na kifaa hicho cha kupeperushia masafa ya GSM, kwani inachangamoto tele za kungamua masafa.
Matumizi ya nguvu zaidi ya shughuli zingine yanaweza kubaiishwa na ''alogarithm'' muundo msingi wa simu yenyewe.
Watafiti hao sasa wameunda mfumo ambao unakusanya habari kuhusu matumizi ya betri ya simu.
‘’Mfumo huo hairuhusu kutumia GPS wala huduma zozote kwa mfano mtandao wa Wi-fi ‘’
Jopo hilo linajumuishwa Yan Michalevsky, Dan Boneh na Aaron Schulman kutoka idara ya sayansi ya tarakilishi katika chuo kikuu cha Standford pamoja na Gabi Nakibly kutoka kwa kampuni ya Rafael waliandika katika utafiti wao.
Utafiti umebaini kuwa betri za simu za android zinawezakutumika kufuatilia watumizi
‘’Tunaruhusa ya kuunganisha mtandao na upatikanaji wa nguvu yao.’’
‘’Hizi ni ruhusa za kawaida kwa mfumo huo na inawezekano wa kutoleta hutuma kwa upande wa mwathiriwa.
Kuna mifumo 179 ambazo zinapatikana kwenye Anaroid ,timu hiyo iliongezea.
Shughuli kama kuskiza muziki au kutumia mtandao wa kijamii inamaliza betri ya simu lakin i hii inaweza kupunguzwa kutokana na ‘’kujifunza kwa mashine’’ripoti inasema.
Jaribio hilo lilifanyiwa kwa simu ambazo zinatumia mtandao wa 3G lakini haikuweza kupima nguvu kwa kuwa twakimu inalindwa na kifaa hicho.
CHANZO BBC.

IS YAWATEKA WAKRISTU 90 SYRIA.

 
 Jamii ya wakristu nchini Syria
Kundi la Islamic State limewateka nyara watu 90 wa jamii ya wakristo kutoka katika kijiji kimoja kazkazini mwa Syria.
Kisa hicho cha utekaji nyara kilifanyika mapema leo alfajiri, baada ya wanamgambo hao kuchukua udhibiti wa vijiji kadhaa kutoka kwa walinda usalama wa kabila la Wakurdi.
Wanamgambo hao walivamia kituo cha Radio na kuchukua udhibiti wa mawasiliano na kuanza kutangaza Radioni, kuwa wamewateka nyara wale wanaojiita watetezi wa Dini.
Kwa muda mrefu kundi la wakristo wachache walioko Nchini humo limekuwa likishirikiana na wapiganaji wa kabila la Wakurdi kukabiliana na wanamgambo wa IS.
Jamii ya wakristu nchini Syria
Awali Kundi la I S limekuwa likiharibu makanisa ya wakristo Nchini Syria.
Wakristo hao wa makabila ya Assyria ambao wengi wamo serikalini, wanaiunga mkono utawala wa sasa wa Syria na wamekuwa wakipigana na wanamgambo hao wa Islamic State.
Idadi ya Wakristo katika maeneo hayo imepungua kwa kasi mno kutokana na mauwaji dhidi yao.
CHANZO BBC.

WAETHOPIA 100 WAKAMATWA KENYA.


Wahamiaji haramu kutoka Ethiopia waliofikishwa mbele ya mahakama Kenya 
Raia wa Ethiopia 100 wamekamatwa nchini Kenya katika mitaa ya mji mkuu Nairobi wakielekea Afrika Kusini.
Polisi wanasema kuwa walipitia Kenya kinyume cha sheria wakitumia mabasi tofauti lakini wakakamatwa wakipumzika katika makazi fulani viungani mwa jiji.
Wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hapo Kesho.
Ni wakimbizi hao walipoletwa hii leo katika mahakama ya Makadara kufunguliwa mashtaka ya kuwa nchii kinyume cha sheria hali kadhalika bila vibali.
Walifika mahakamani wengi wao wakiwa wachovu kutokana na safari ndefu kutoka Ethiopia na kwa kukosa chakula.
Mmoja wao alikuwa taabani hadi hakimu akasema apelekwe hospitalini ama apewe chakula.
Wengine walinong’ona kuwa wanahisi njaa.
Hata hivyo walipoulizwa ikiwa wanaweza kuzungumza Kingereza walikana japo wakakiri kuwa wanakielwa tu kiamariki lugha asilia ya Ethiopia.
Kutokana na hali hiyo hakimu aliagiza warejeshwe korokoroni kisha wafikishwe Mahakamani hapo Kesho atakapopatikana mkalimani anayeelewa lugha yao.
 Wahamiaji haramu kutoka Ethiopia waliofikishwa mbele ya mahakama Kenya
Kwa mujibu wa polisi washukiwa hao walikuwa safarini kuelekea Afrika Kusini japo walipata ugumu wa kujieleza zaidi kutokana na matatizo ya lugha.
Hii si mara ya kwanza raia wa kigeni kupatikana Kenya wakiwa safarini kuelekea mataifa mengine kujitafutia ajira ama kuwa wahamiaji katika nchi wanazodhania kuwa zitawafaa kwa ajira na maslahi mbalimbali.
Kadhalika kuna dhana kuwa wengine hutumiwa na wafanyibiashara wanaolangua watu.
Mwaka wa 2012 raia wa Ethiopia 42 walipatikana wamefariki katika lori lilokuwa limefunikwa kila mhali kwa kukosa hewa.
Ilisemekana kuwa raia hao vile vile walikuwa wakielekea Afrika Kusini mojawepo ya nchi ambazo ziajulikana kwa kuwa na wahamiaji wengi.
CHANZO BBC.