Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 13 Februari 2015

FEDHA ZA KUKABILIANA NA EBOLA ZATOWEKA.

 
Ebola nchini Sierra leone 
Ripoti moja imebaini kwamba karibia dola millioni 14 za kugharamia vita dhidi ya ebola nchini Sierra Leone hazijulikani zilipo.
Mkaguzi mkuu amesema kuwa wizara ya afya na kituo cha kitaifa cha kukabiliana na ugonjwa wa ebola zilienda kinyume na sheria.
Mkaguzi huyo amesema kuwa taasisi hizo mbili zilishindwa kutoa stakhabadhi za kandarasi zilizotolewa kununua ambulansi na kujenga kituo cha matibabu ya ebola .
Ripoti hiyo imesema kulikuwa na malipo ya dharura mara mbili kwa wabunge na maafisa wa polisi na kwamba fedha zilipewa watu fulani badala ya mashirika ambayo wangewakilisha.
Serikali haitoa jibu lolote kuhusu ripoti hiyo.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni