Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 26 Februari 2015

BENSOUDA AWASILI UGANDA ,KUNANI

 
 Mwendesha mashtaka mkuu katika mahakama ya ICC Fatou Bensouda
Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC Fatou Bensouda amewasili nchini Uganda ili kutafuta ushahidi kuhusu kesi ya aliyekuwa kamanda mkuu wa wapiganaji wa LRA nchini Uganda .
Dominic Ongwen ambaye alisema alitekwanyara na LRA akiwa mtoto alifikishwa mbele ya mahakama ya ICC mjini Hague mnamo mwezi Januari akikabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kivita.
Mwandishi wa BBC mjini Kamapala anasema kuwa Bensouda atazuru kazkazini mwa Uganda katika ziara ya siku tano ili kuzungumza na mashahidi mbali na kutembelea maeneo yaliotekelezewa uhalifu huo.
Pia anatarajiwa kukutana na rais Yoweri Museveni wa Uganda ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa mahakama hiyo ya ICC akiishtumu kwa kuwabagua viongozi wa Afrika.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni