Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 13 Februari 2015

MAPIGANO KUSITISHWA JUMAMOSI UKRINE.



Viongozi wa mataifa ya Ulaya katika mkutano wa makubaliano kusitisha mapigano Ukraine
Viongozi wa mataifa ya Ulaya wamesema kuwa wataiwekea vikwazo zaidi Urusi iwapo itashindwa kusimamia makubaliano mapya yaliyofikiwa kusitisha mapigano Mashariki mwa Ukraine.
Kansela wa Ujeruman Angela Merkel amesema kuwa tayari mataifa hayo yalishakubaliana vikwazo hivyo itakavyo wekewa Urusi iwapo itakiuka makubaliano hayo. Markel aliyasema hayo muda mfupi baada ya viongozi hao wa Ulaya kuwasilisha makubaliano yanayo zihusisha Ukaraine na Urusi kufuatia machafuko yanayoendelea. Usitishaji wa mapigano mashariki mwa Ukraine unatarajiwa kuanza rasmi Jumamosi usiku,hata hivyo wanajeshi wa Ukraine na Waasi wa Urusi wapo katika hali ya wasiwasi kufuatia makubaliano hayo mapya huku kila upande ukiangalia mwingine katika utekelezaji wa kuelekea kuleta Amani mashariki mwa Ukraine.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni