Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 11 Februari 2015

NGO DRC ZATAKA MUNUSCO ISIJIONDOE CONGO.


Majeshi ya kulinda amani MUNUSCO yaliyopo Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo 
Mashirika mbali mbali ya kiraia nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yameomba majeshi ya Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini humo MUNUSCO kufikiria upya mpango wake kujiondoa kupambana na kundi la waasi la FDLR.
Hapo jana majeshi ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa yaliyopo Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo yalitangaza kujiondoa katika operesheni hiyo kwa kushirikiana na majeshi ya serikali ya DRC hadi hapo serekali ya Kongo itakapotengua uteuzi wa majenerali wawili walioteuliwa kuongoza opereshini hiyo.
Kwa mujibu wa MUNUSCO majenerali hao wana tuhumiwa kufanya vitendo vya ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni