Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 23 Februari 2015

MISRI YAMHUKUMU MWANDISHI MIAKA 5 JELA.


Mahakama nchini Misri imemhukumu Alaa Abdel Fattah kifungo cha miaka 5 gerezani 
Mahakama moja mjini Cairo Misri imemhukumu mwandishi wa blogu kifungo cha miaka 5 jela kwa kukiuka sheria za undamanaji
Mahakama hiyo ilimpata na hatia mwanablogu Alaa Abdel Fattah, kwa mchango wake katika maandamano na mapinduzi ya serikali mwaka wa 2011.
Majaji walimpata na hatia ya kukiuka sheria zinazosimamia undamaji nchini humo.
Kauli hiyo ni kama msumari kwenye kidonda kwa Alaa Abdel Fattah ambaye alikuwa ameachiliwa kwa
dhamana na mahakama nyengine nchini mwaka uliopita baada ya kukata rufaa ya kifungo cha miaka 15 jela.
Alaa Abdel Fattah alijipatia sifa baada ya kuwa mstari wa mbele kupinga udhalimu uliokuwa ukiendelezwa na
Mahakama nchini Misri imemhukumu Alaa Abdel Fattah kifungo cha miaka 5 gerezani
utawala wa aliyekuwa rais wa muda mrefu nchini humo Hosni Mubarak.
Hii ilikuwa dalili mbaya kwa waandishi wa habari wa shirika la utangazaji la Al-Jazeera, Mohamed Fahmy na Baher Mohamed
ambao walirejea leo mahakamani kwa kusikizwa kwa kesi dhidi yao.
Hata hivyo kesi dhidi yao iliahirishwa hadi Machi tarehe 8 kwa mujibu wa shirika la habari la Associated Press
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni