Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 28 Februari 2015

MAREKANI KUFUNGUA UBALOZI WAKE CUBA.

 
 Rais Obama
Marekani inasema kuwa itafungua ubalozi wake nchini Cuba kuanzia mwezi Aprili.
Baada ya duru ya pili ya mazungumzo mjini Washington yenye lengo la kurejesha uhusiano kati yao mwanadiplomasia wa cheo cha juu wa Marekani katika nchi za Marekani ya kusini Roberta Jacobson, alisema kuwa itawezekana kufunguliwa kwa ubalozi kabla ya mkutano wa kimaeneo ambao utafanyika nchini Panama kuanzia tarehe kumi mwezi Aprili.
Mkuu wa ujumbe wa Cuba Josefina Vidal alisisitiza kuwa Marekani ni lazima iondoe Cuba kutoka kwa orodha ya nchi ambazo zinaunga mkono Ugaidi kabla ya kurejesha tena uhusiano huo.
Mwezi Disemba Cuba na Marekani walitangaza kuwa walikubaliana kuboresha uhusiano wao baada ya zaidi ya miaka 50 .
chanzo bbc.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni