Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 10 Februari 2015

MAPIGANO BADO YANAENDELEA MASHARIKI MWA UKRAINE



Raia wakishangaa mamshambulizi yaliyofanywa huko mashariki mwa Ukraine,kufuatia mapigani yanayoendelea huko. 
Mapigano makali yameendelea mashariki mwa Ukraine kufuatia majeshi ya serikali kukabiliana na kundi la Waasi wanaodaiwa kuungwa mkono na Urusi.
Raia wanane na wanajeshi wanne wameuawa kufuatia mashambulizi ya silaha kati ya majeshi ya serikali na Waasi katika mji wa Kramatorsk unaoshikiliwa na serikali.
Hata hivyo mapigano hayo yanakuja huku kukiwa na mpango wa mazungumzo ya amani ili kusitisha mapigano hayo. Vyombo vya habari nchini Urusi vinasema makubaliano ya muda ya kusimamisha mapigano yamefikiwa, japo kuwa hakuna uthibitisho wa serikali. Mapambano bado yanaendelea katika mji wa Debaltseve na wanajeshi wa serikali wa Ukraine wamefanya mashambulizi dhidi ya waasi mashariki mwa Mariupol.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni