Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 17 Februari 2015

MISRI YATAKA UN KUISHAMBULIA ISIS LIBYA

 
Rais Abdel Fattah el-Sisi wa Misri akiwafariji wakuu wa Kanisa la Coptic 
Akizunguma na kituo kimoja cha radio cha Ufaransa ( Europe One) rais Sisi alisema kuwa watu nchini Libya wanataka hatua kali kuchukuliwa ili kuleta usalama na udhabiti nchini mwao.
Al sisi alisema ''Hatutawaruhusu watoto wetu wachinjwe ovyo na hawa magaidi.''
Wito wa rais Sisi unakuja siku moja baada ya ndege za kivita za Misri kushambulia ngome za Islamic State kulipiza kisasi kuuawa kwa wamisri wa dhehebu la Coptic nchini Libya siku ya Jumamosi.
Hapo jana , Taarifa kutoka Misri zilisema kuwa, ndege za kijeshi ziliwashambulia wapiganaji wa jihadi nchini Libya kwa mabomu, baada ya kutolewa kwa mkanda wa video ulioonyesha wakristo wa Misri wa madhehebu ya Coptic
Misri yataka UN kuingilia kati Libya kuzuia kuenea kwa ISIS
wakikatwa shingo.
Jeshi la Misri lilisema kuwa lililenga kambi za Islamic State, kituo cha mafunzo na maghala ya silaha, katika shambulizi hilo la mapema leo alfajiri.
Walioshuhudia wanasema kuwa, mji wa Derna ulioko mashariki mwa Libya na ambao umetekwa na wapiganaji wa jihadi ndio ulioshambuliwa vibaya.
Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi, alisema kuwa mashambulio hayo ya angani ni jibu kwa wapiganaji hao ambao walitoa mikanda hiyo ya video hapo jana jumapili ilionyesha waumini kumi kati ya 21 waliotekwa nyara wakichinjwa.
 Ndege za kijeshi baada ya kutekeleza mashambulizi Libya
Waumini hao wa madhehebu ya Coptic walikuwa wametekwa nyara majuma kadha yaliyopita.
Jeshi la Misri lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari ikisema kuwa raia wa taifa hilo walioko mbali ama karibu, wanafaa kuelewa kuwa wanajeshi la taifa linalowalinda kokote waliko.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni