Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 26 Februari 2015

BANGI NI HALALI WASHINTON DIC.

 
 Mji mkuu wa Marekani Washington DC umehalalisha utumizi wa Bangi
Mji mkuu wa Marekani Washington DC umehalalisha utumizi wa Bangi.
Hatua hii ya Washington inafuatia ile ya jimbo la Colorado, Alaska na Washington state ya kuhalalisha matumizi ya mihadarati kwa starehe.
Mpango huo umekubalika na wananchi wengi katika kura ya maoni iliyopigwa Novemba mwaka jana lakini maafisa nchini
humo wametofautiana na wabunge wa Republican ambao ni wengi bungeni uliosababishwa kusitisha eneo hilo kuidhinisha mbinu za kudhibiti na kutoza kodi mhadarati huo.
Sheria hiyo mpya itaanza kutumika kuanzia saa tano usiku wa Alhamisi na hivyo mtu yeyote atakayekuwa akimiliki bangi kisiri atakuwa huru kuivuta bila hofu ya kukamatwa..
Sheria hiyo mpya hata hivyo imezua tofauti baina ya Meya wa mji huo na bunge la Congress.
Weneyji wa mji huo wenye umri unaozidi miaka 21 watakuwa huru kumiliki gramu 56 ya Bangi.
 
Meya wa Washington Muriel Bowser
Aidha wanauwezo wa kuipanda majumbani mwao.
Hata hivyo sheria hiyo mpya inaharamisha kuuzwa kwa bangi na ununuzi wake.
Mji mkuu wa Washington DC - ni wilaya maalum lakini haina uhuru na hadhi sawa na majimbo kwa hivyo kuna dhana kuwa ilikiuka kanuni ilipoamua kupiga kura ya maoni.
Katika Barua iliyoandikwa na wajumbe wa bunge hilo la Congress,Meya wa Washington Muriel Bowser ameonywa kuwa sheria za jimbo zinakiukwa iwapo sheria hiyo maarufu itaanza kutekelezwa.
Wajumbe hao wanadai kuwa kulingana na sheria maalum iliyopitishwa na Bajeti ya taifa Kuhalalishwa kwa bangi ni haramu.
Bi Bowser hata hivyo anaendelea kushikilia kukutu kuwa walifwata kanuni zote zilizowekwa.
CHANZO  BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni