Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 28 Februari 2015

KIONGOZI WA UPINZANI AUAWA URUSI.

 
Maafisa wa polisi wakiweka usalama katika eneo ambalo kiongozi wa upinzani nchini Urusi Boris Nemtsov aliuawa 
Mmoja wa wanasiasa maarufu wa upinzani nchini Urusi Boris Nemtsov ameuawa kwa kupigwa risasi kwenye mji mkuu wa nchi hiyo Moscow.
Mwanasiasa huyo alipigwa risasi nne kutoka nyuma na watu waliokuwa ndani ya gari alipokuwa akitembea nje ya makao makuu ya serikali.
Bwana Nemtsov ambaye alihudumu kama naibu waziri mkuu wakati wa uongozi wa rais Boris Yeltsin alikuwa akimshutumu vikali rais Vladimir Putin.
 
Boris Nemtsov
Alikuwa akipanga mkutano ambao ungefanyika kesho Jumapili kupinga kile alichokitaja kuwa vita vinavyoendeshwa na Urusi nchini Ukrain.
Kwenye mahojiano mapema mwezi huu bwana Nemtsov alisema kuwa alikuwa na hofu kuwa rais Putin angemuua.
CHANZO  BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni