Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 17 Februari 2015

MAAFISA POLISI 20 WAUAWA AFGHANISTAN

 
 Wanamgambo wa Taliban wamekuwa wakihatarisha usalama wa Afghanistan
 Maafisa Mashariki mwa Afghanistan wamesema maafisa wa Polisi 20 wameuawa katika mashambulio kadhaa.Watu wanne wameripotiwa kuvalia mavazi ya Polisi na kuingia katika Ofisi za makao makuu ya Polisi katika jimbo la Logar, na kujilipua.
Gavana wa Jimbo hilo Niaz Muhammad Amiri ameiambia BBC kuwa Maafisa wengine wanane walijeruhiwa.Wengi kati ya waliopoteza maisha walikuwa wakipata chakuwa wakati wa mapumziko.
Kumekuwa na ongezeko la mashambulizi ya Wanamgambo miezi ya hivi karibuni wakati ambapo vikosi vya usalama vikiwa vimechukua udhibiti wa nchi hiyo kutoka kwa Majeshi ya NATO.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni