Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 4 Februari 2015

230 WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA MISRI


Maandamano ya Mwaka 2011 yaliuangusha utawala wa Hosni Mubarak
Mahakama nchini Misri imetoa hukumu ya kifungo cha maisha dhidi ya Watu 230 akiwemo mmoja kati ya Wanaharakati vinara walioongoza harakati za kuuangusha utawala wa Hosni Mubarak kwa makosa ya kushiriki katika maandamano dhidi ya Serikali ya Cairo miaka mitatu iliyopita.
Mwanaharakati Ahmed Douma pia ametozwa faii ya Dola milioni 2.2 kwa kosa la kuchoma moto taasisi ya mafunzo ya Sayansi.
Kesi hiyo ilihusishwa na mapigano nje ya majengo ya wizara jijini Cairo mwezi Desemba mwaka 2011.
Miongoni mwa mashtaka yanayomkabili ni pamoja na kuwashambulia Maafisa usalama na kuvamia ndani ya Jengo la Wizara ya mambo ya ndani.
Kwa kosa hilo Douma kwa sasa anatumikia kifungo cha miaka mitatu.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni