Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 4 Februari 2015

JORDAN YAAPA KUPAMBANa NA ISLAMIC STATE


Mfalme Abdullah wa Jordan
Mfalme wa Jordan ameahidi mapambano yasiyo na huruma dhidi ya wapiganaji wa Islamic State kufuatia kuuawa kwa rubani wa nchi hiyo.
Baada ya mkutano wa makamanda wa juu wa jeshi na maafisa usalama, Mfalme Abdullah amesema vita hivyo vitaelekezwa dhidi ya kundi hilo na damu ya rubani huyo wa ndege za kivita Muath al-Kasasbeh haitapotea bure.
Hapo jana, Jordan iliwanyonga wafungwa wawili wapiganaji wenye msimamo mkali waliokuwa katika orodha ya adhabu ya kifo, kama kulipiza kisasi cha kuuawa kwa rubani wake huyo.
Miongoni wa walionyongwa ni Sajida Al-Rishawi, ambaye wapiganaji wa Islamic State walitaka aachiwe kama sehemu ya kubadilisha na mateka huyo wa Jordan waliokuwa wakimshikilia.
Katika hatua nyingine kundi la wabunge wa Uingereza limeitaka nchi yao kuchukua hatua zaidi kupambana na kundi hilo la Islamic State.
Ripoti kali iliyotolewa na kamati ya Ulinzi ya bunge hilo imesema maafisa na maafisa waandamizi wa jeshi wameshindwa kuanzisha mikakati iliyowazi kufikia malengo ya kuwashinda wapiganaji hao wenye msimamo mkali.
Awali serikali ya Uingereza ilisema hatua zinazochukuliwa za kutoa msaada wa kijeshi ni moja ya sehemu ya mikakati ya ulimwengu kupambana na kundi hilo.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni