Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 5 Februari 2015

BOBBI KRISTINA BADO YUKO HOSPITALINI.



Bobbi Kristina akiwa na Mama yake Marehemu Whitney Houston 
Wakati Bobbi Kristina akiwa bado Hospitalini, Mwanasheria wa Baba yake amesema kwa sasa wanafanya uchunguzi kubaini kilichomsababishia Bobbi Kristina kulazwa.
Mwanasheria Christopher Brown amesema Mtoto wa waimbaji Marehemu Whitney Houston na Bobby Brown hakuwahi kuolewa na Nick Gordon kama ambavyo ripoti kadhaa zimekuwa zikidai.
Bobbi Kristina Brown alikutwa akiwa amepoteza fahamu akiwa bafuni mwishoni mwa juma. Familia yake imekuwa kimya kuhusu hali yake, lakini Baba yake alitoa taarifa kupitia mwanasheria wake siku ya jumanne.
Bobby Brown ameomba jamii iache ishughulikie mambo ya kifamilia kwa uhuru na kumuonesha upendo bintiye.
Binti huyo alifikishwa hospitalini baada ya kugundulika kuwa hakuwa na fahamu hali iliyowafanya kumkimbiza hospitali, mpaka siku ya jumatatu jioni alikuwa bado kwenye chumba cha wagonjwa mahututi.
Siku ya jumanne alihamishiwa kwenye Hospitali ya Chuo cha Emory mjini Atlanta, Vyanzo vilivyo karibu na Familia ya Brown vimeeleza.
chanzobbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni