Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 5 Februari 2015

KUNAWA MIKONO IWE HIARI BAADA YA KUTOKA MALIWATO


Kazi ya kunawa mikono iwe hiari binafsi
Seneta mmoja nchini Marekani amewataka wamiliki wa migahawa nchini humo kuacha tabia ya kuwashurtisha wafanyakazi wao kunawa mikono baada ya kutoka maliwatoni.
Seneta Thom Tillis, wa chama cha Republican kutoka North Carolina ,ametoa kauli hiyo mapema wiki hii wakati alipokuwa akipinga kanuni za biashara na kuwataka wafanyakazi waachwe waamue wenyewe kuosha mikono yao, ama lah.
Kauli ya seneta huyo imekuja baada ya kanuni kuelekeza kuwa mgahwa ambao hautawaelekeza wafanyakazi wake kunawa mikono,waache kufanya biashara haraka.
Seneta Tills, akashauri kuwa migahawa ambayo wafanyakazi wake hawanawi mikono wanapaswa kuweka alama wazi kwa wateja wao kama ishara ya utaratibu wao,kauli hii ya pili Tillis aliitoa wakati wa mahojiano na Us Capitol.
Tills akatetea hoja yake kwamba, Kuna wakati zipo kanuni ambazo pengine tunahitaji kuzipa muelekeo,lakini waachi wale ambao wamewekewa kanuni hizo hiyo waamue kama ina leta maana ama lah na wafanye maamuzi hayo kinyume na serikali.
Hoja hii imekuja huku wagombea uraisi walio wengi kutoka katika chama cha Republican,wakiamini kwamba wataulizwa maswali kuhusiana na kanuni na taratibu za chanjo ya ugonjwa hatari wa Ebola
Walau wazazi wawili wao wameonesha msimamo wa dhahiri kuwa wakati mwingine huwataka watoto wao kuikwepa chanjo hiyo pindi wanapohudhuria masomo yao.
chanzobbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni