Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 5 Februari 2015

GHASIA ZAZUKA GEREZANI GHANA



Vurugu zililazimu Polisi kuongeza nguvu ili kudhibiti Wafungwa 
Mtu mmoja ameuawa na wengine wanne kujeruhiwa katika mapigano yaliyotokea katika Gereza moja mjini Kumasi nchini Ghana wakati Wafungwa walipokuwa wakijaribu kutoroka wakati ilipotokea ajali ya moto.
Maafisa wa usalama walipambana na Wafungwa, hali iliyosabisha mfungwa mmoja kupoteza maisha Polisi wanne walijeruhiwa.
Wafungwa hao walikuwa wakijaribu kutoroka wakati walipokuwa wakihamishwa kutoka kwenye vyumba vyao wakati moto ulipotokea.
Moto huo unaelezwa kutokea baada ya kuwepo hitilafu kwenye Taa.
Polisi walilazimika kutumia gesi za kutoa machozi dhidi ya wafungwa hao ambao walikuwa wakiwarushia fimbo, mawe na viti.
Msemaji wa Gereza la Kumasi James Annan amesema pamoja na vurugu hizo hakuna Mfungwa yeyote aliyeweza kutoroka.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni