Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 5 Februari 2015

HALI YA MASHARIKI MWA UKRAIN NI TETE.


Mapigano yanayoendelea yameeathiri Wakazi wa Debaltseve
Shirika lijihusishalo na maswala ya usalama na ushirikiano barani Ulaya,OSCE limesema hali ya Mashariki ya Ukraine inazidi kuwa mbaya na mashambulizi dhidi ya Raia yanazidi kuongezeka.
Msemaji wa OSCE,Shirika linafuatilia hali ilivyo nchini Ukraine amesema silaha zilizopigwa marufku kimataifa zilitumika juma lililopta katika mji unaoshikiliwa na waasi Luhansk.
Amesema mabomu ambayo yalipigwa marufuku kutumika kwenye maeneo ya Watu wengi chini ya Sheria za kimataifa yamesababisha madhara kwa Raia na kuharibu mali zao.
Baadae hii leo, Mkuu wa Shirika la OSCE atahutubia Baraza lake la kudumu, anatarajiwa kutoa wito wa kusitisha mapigano kwa muda katika Mji unaodhibitiwa na Serikali wa Debaltseve ambao mapigano yameongezeka Wiki za hivi karibuni.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni