Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 2 Februari 2015

MWEZI MMOJA TOKA MAUJI YA BAGA NIGERIA


Mji wa Baga ulioshambuliwa na Boko Haram
Leo ni mwezi mmoja tangu wapiganaji wa Boko Haram waliposhambulia miji ya Baga na Doron Baga kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Idadi kamili ya watu waliokufa haijulikani lakini inadaiwa kuwa ni kati ya watu mia moja na hamsini hadi elfu mbili.
Wakati wapiganaji wa Boko Haram wakivamia kutoka upande wa magharibi wa Baga, kundi la vijana waliodhamiria kupambana na kundi hili walijaribu kuulinda mji wao.
Yalikuwa mafanikio ya nadra kutokea dhidi ya Boko Haram. Kulikuwa na ahueni lakini haikudumu muda mrefu.
Ilikuwa taharuki. Wanawake na watoto, vijana na wazee walizikimbia nyumba zao na biashara, wengi wakikimbilia mji jirani wa uvuvi wa Doron Baga ulio ufukweni mwa Ziwa Chad.Boko Haram waliwafuata Doron.
Iwapo bunduki haikukudhuru, walianza kuua watu kwa kuwagonga na magari yao. Ufyatuaji wa risasi haukuchagua pa kulenga
Mauaji ya Baga na Doron Baga yalitokea mwezi mmoja uliopita…Boko Haram hawakusambaratishwa. Tangu wakati huo, waasi hao wameishambulia miji mingi zaidi kaskazini mashariki mwa Nigeria; watu wengi wamekufa na wengi zaidi wamelazimika kuyakimbia makazi yao.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni