Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 7 Februari 2015

SULUHU HUENDA ISIPATIKANE UKRAINE.

Rais wa Ukraine Poroshenko aonesha pasi za wanajeshi wa Urusi, kuonesha kuwa wako Ukraine mashariki
Makamo wa rais wa Marekani, Joe Biden, amesema Marekani iko tayari kuisaidia Ukraine kujihami dhidi ya wapiganaji wanaosaidiwa na Urusi.
Akizungumza kwenye mkutano mjini Munich, Ujerumani, kuhusu usalama wa Ukraine, Bwana Biden alisema Marekani inataka suluhu ya amani katika mzozo wa Ukraine.
Lakini alisema mara nyingi Rais Putin ameahidi amani huku akiendelea kuwapatia wapiganaji wanajeshi, vifaru na silaha.
Hapo awali, kiongozi wa Ujerumani, Angela Merkel, alionya kuwa Ukraine isipatiwe silaha - lakini alisema hakuna hakika kuwa juhudi za sasa za kutafuta amani zitafanikiwa.
Rais Putin amekanusha kuwa Urusi inataka vita - lakini kwa mara nyegine tena amelalamika juu ya vikwazo vilivowekwa na mataifa ya magharibi dhidi ya nchi yake.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni