Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 4 Februari 2015

VIKOSI VYA CHAD VYAWAUA WAPIGANAJI 200


Wanajeshi wa Chad
Jeshi la Chad linasema kuwa limewaua wapiganaji 200 wa kundi la boko Haram huku nao wakipoteza wanajeshi 9 katika vita vikali vya kuuteka mji muhimu kazkazni mashariki mwa Nigeria.
Wapiganaji wa Boko Haram waliwauwa watu 30 baada ya kutoroka mapigano hayo na kuelekea nchini Cameroon,mkaazi mmoja amesema.
Vilikuwa vita vikali vilivyowahusisha wapiganaji wa Chad tangu waingie Nigeria ili kukabiliana na wanamgambo hao.
 Chad
Vikosi vya Chad na vile vya Cameroon pia vinaendelea kuangusha mabomu katika msitu mkubwa wa sambiza ambapo wapiganaji hao wana kambi.
Boko Haram wanadaiwa kutorokea katika katika msitu huo baada ya kuwateka zaidi ya wasichana 200 wa shule mnamo mwezi Aprili kutoka mji wa kazkazini mashariki mwa Nigeria wa Chibok.
Haijulikani iwapo bado washichana hao wapo katika msitu huo.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni